Wednesday, September 29, 2010

KATA YA MWANANYAMALA WAMPOKEA KWA KISHINDO MH:IDDI AZZAN.


Mh:Iddi Azzan akimnadi Mgombea Udiwani Ndugu Songoro Mnyonge kwa wananchi wa kata ya Mwananyamala wa kati wa kampeni zilizofanyika hapo jana, aliwaomba wananchi wachague Viongozi wa chama cha Mapinduzi kwa Maisha bora ikiwa nafasi ya Urais Mh:Jakaya Kikwete, Ubunge kwa Jimbo la Kinondoni yeye Mwenyewe Mh:Iddi Azzan na Kata hiyo ya Mwananyamala nafasi ya Udiwani Ndugu Songoro Mnyonge.
Mh:Iddi Azzan Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni akiwa amekaa pamoja na Mgombea Udiwani Ndugu Songoro Mnyonge wakati wa kampeni zilizofanyika kata ya Mwananyamala.
Mh:Iddi Azzan akiwapungia mikono wananchi wa kata ya Mwananyamala wakati akiwasili katika uwanja wa kampeni uliopo katika kata hiyo.
Wananchi wa kata ya Mwananyamala wakimpokea Mh:Iddi Azzan alipokuwa anawasili katika uwanja wa kampeni katika kata hiyo.

Monday, September 27, 2010

Wanachama 34 kutoka CHADEMA na Mmoja Kutoka CUF wajiunga na CCM wakipokewa na Mh:Iddi Azzan,Kinondoni shamba.


Mh:Iddi Azzan awapongeza wanachama waliorudisha kadi na kukubali kuwa chama cha Mapinduzi ndio chama kinacho stahiki kupewa kura na kuendelea kuiongoza Tanzania kwa sera zake za maendeleo. pia alisema atahakikisha anisimamia sheria ya watoto  ya mwaka (2009) kuwa watoto lazima wapewe haki zao zote za msingi. Mwisho aliendeleae kutilia mkazo wananchi wasifanye makosa tarehe 31 na kuwataka waachague mafiga matatu yote ya CCM.
Mh:Iddi Azzan akimnadi Mgombea Udiwani Bi Husna na kuwaomba wananchi wampe kura ili waweze kushirikiana na yeye katika kuleta maendeoleo ya kata hiyo.
Kadi zilizorudishwa na wanachama 35 kutoka Chama Cha CHADEMA na Mmoja akitokea CUF. katika uwanja wa kampeni wa kinondoni Shamba.
 Mh:Iddi Azzan akimkabidhi nguo za CCM Ndugu Mgendi baada ya kurejesha kadi yake ya CHADEMA.
Mh:Iddi Azzan akimpa nafasi ya kujielezea Mwanachama aliyerejesha kadi ya chama cha CHADEMA na kuhamia chama cha Mapinduzi hapo jana katika uwanja wa kinondoni shamba.
 Mh:Iddi azzan akiwa na mjuu kuu wa Mgombea udiwani Bi husna. ambaye amekaa upande wakushoto.
Wasanii wa Wafataki wakitoa burudani kwa wananchi wa kinondoni shamba
Kikundi cha Mizengwe ambacho kinashugulika na maswala ya uigizaji, wa kifanya igizo fupi katika uwanja wa mkutano wa kampeni.

Mtoto mdogo akionyesha kipaji chake cha kucheza mbele ya Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi. katika uwanja wa kampeni wa kata ya kinondoni.
Wananchi wakiwa wamefurika katika uwanja wa kampeni kinondoni shamba.
Wananchi pamoja na makada wa CCM wakiwa wamenyosha mikono wakiashiria kukubali kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi.

Mh:Iddi Azzan awaomba wananchi wa kata ya Kijitonyama wamchague yeye katika nafasi ya Ubunge na wamchague Diwani Bulembo pamoja na Mh:JK katika nafasi ya Urais.

Mh:Iddi Azzan mgombea Ubunge Jimbo la kinondoni akiwa amekaa pamoja na Mgomea Udiwani wa kata ya kijitonyama.
Mh:Iddi Azzan akiwapungia mkono wa salamu wananchi wa kata ya Kijitonyama katika Mkutano wa kampeni uliofanyika Alimaua kata ya Kijitonyama. aidha aliwataka wananchi wamchague yeye mwenyewe katika nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kinondoni na wamchague Mgombea udiwani wa chama cha Mapinduzi Ndugu Bulembo Abdallah  ili waendeleze yale waliokuwa hawayajamaliza katika kipindi kichopita. pia aliwaomba kumpigia kura Mh: Jakaya Kikwete kwa kuwa ni rais mwenyesifa na vigezo vyote vyakuendelea kuiongoza nchi hii.
Mgombea Udiwani Ndugu Bulembo akieleza sera zake kwa wananchi wa kata ya Kijitonyama na kuwataka wachague mafiga matatu.
Mh: Mgeni rasmi ndugu Msabah akiwaombea kura Wagombea wa Chama Cha Mapinduzi ikiwa ni Mgombea Ubunge Mh:Iddi Azzan na Mgombea Udiwani Ndugu Bulembo Abdallah pamoja na Mgombea Urais Mh:Jakaya Mrisho Kikwete. katika uwanja wa Alimaua, kata ya Kijitonyama.
Wananchi walikuwa wengi sana.


Friday, September 24, 2010

JK, IDDI AZZAN NA MUTAYOBA WAPIGIWA DEBE NA MTOTO CHIPUKIZI, MWANANYAMALA KATA YA MAKUMBUSHO.

Mh:Iddi Azzan na Mutayoba wakiwapungia mikono wananchi wa Makumbusho katika uwanja wa Kampeni wa kata hiyo.
Wananchi wa kata ya Makumbusho wakisikiliza kwa makini sera za wagombea wa chama cha CCM walipokuwa wakinadi sera zao katika uwanja wa kampeni wa kata hiyo.
Mh:Iddi Azzan akitoa sera zake kwa wanachama wa kata ya Makumbusho akiwaambia kuwa watoto atawapa kipa umbele kuhakikisha wanapata haki zote za msingi.
Mtoto Chipukizi Mohamed akiwapigia debe Viongozi wa CCM na kusema kuwa Vyama pinzani havina nafasi.


Wednesday, September 22, 2010

MH:IDDI AZZAN, CHENGULA PAMOJA NA JK HAWANA MPINZANI KATA YA KIGOGO!!!

Mh: Iddi Azzan akiwaeleza sera zake wananchi wa kata ya Kigogo katika uwanja wa kigogo mwisho uliopo katika kata hiyo, mkutano huo ulikuwa wa aina yake kwa siku ya jana.
Mwenyekiti wa Jimbo la Kinondoni Mzee Sisiyamoto akiwaombea kura Viongozi wote wa chama hicho pamoja na Kumtambulisha Mgombea Ubunge Mh: Iddi Azzan na Mgombea Udiwani Ndugu Chengula. katika uwanja wa kampeni wa kata ya kigogo.
Mgombea Udiwani ndugu Chengula wa kata ya kigogo akitoa sera zake katika uwanja wa kampeni zilizofanyika katika uwanja wa kigogo mwisho ndani ya kata hiyo ya kigogo.
Mwenyekiti wa Kata ya kigogo akifungua mkutano wa kampeni uliofanyika katika kiwanja cha Kigogo Mwisho ndani ya kata hiyo.
Ndugu Mwinyikheri amabye alikuwa Chama cha CUF Jimbo la Kinondoni sasa arudi tena CCM akiwa hutubia wananchi wa Kigogo, asema kuwa wapinzani ni waongo hawana Mipango ya kuwasaidia wananchi.
Ndugu Maulid Selemani Mkwanju alikuwa katibu wa Vijana Wilaya kinondoni katika chama cha CHADEMA akieleza kwa nini aliondoaka ndani ya chama hicho. na kujiunga na chama cha CCM. asema kuwa viongozi wa chama hicho wote sio waaminifu.
Mgombea ubunge wa Jimbo la Kinondoni Mh: iddi Azzan aliyesimama akiwapungia mikono wananchi kwa dhumuni la kujitambulisha baada ya kikundi kimoja cha wasanii kutaka afanye hivyo. 
Diwani wa kata ya kigogo Ndugu Richard Chengula akipungia mikono wananchi baada ya kuambiwa kufanya hivyo na moja ya kikundi cha wasanii.
Mh: Iddi Azzan Mgombea Ubunge jimbo la kinondoni akiwa na Ndugu Richard Chengula mgomea Udiwani wakiwa wanafurahi kwa pamoja kutokana na vituko vya wasanii.

Wananchi walivyofurika katika mkutano huo wa kampeni huko kata ya kigogo.

Wasanii wamakundi mbalimbali wakiburudisha katika uwanja huo wa kampeni ikiwa pamoja na makundi maarufu kundi la Fataki na Mizengwe. 
Palikuwa hapatoshi waliokaa juu ya nyumba, juu ya magari.
Watoto wakitaka kumsalimia Mh:Iddi Azzan na upande wa kulia Jamaa aliyeshika bango lenye ujumbe kwa jamii na pia amejichora jina la Azzan Kichwani kwake pamoja na la diwani Chengula. 
Umati wa watoto picha ya kushoto wakimzunguka Mh Iddi Azzan wakitaka kumsalimia. na Picha ya kulia ni umati wa watu wakimsindikiza kwenye gari Mh: Iddi Azzan.

Picha ya Kushoto Mgombea Ubunge Mh: Iddi Azzan na Mgombea Udiwani Ndugu Chengula wakiwa katika gari la wazi juu wakiwapungia mikono wannchi wao na Picha ya pili kulia ni wasanii wa Mizengwe wakiwa ndani ya gari na msafara wa Mh: Iddi Azzan wakati wa kuelekea kwenye kampeni.

Iddi Azzan akitoa sera zake katika kata ya tandale

Monday, September 20, 2010

MH:IDDI AZZAN ASEMA TANDALE ITAENDELEA KUJENGWA.

Mh: Iddi Azzan akitoa sera zake kwa wananchi wa kata ya Tandale kwenye uwanja wa Mkunguje, alisema yafuatayo;

1-Aliwaambia kuwa wanashughulikia suala la kujengwa kwa barabara hiyo ya Mkunguje na pia kurekebisha sehemu hiyo kuhusiana na suala zima la maji ya mvua kukaa hapo.

2-Katika suala la huduma ya afya katika kata hiyo teyari tumejenga Zahanati ambayo tunaipandisha hadhi na kuwa hospitali inayotumika kwa ajili ya wananchi wa kata hiyo, pia tumefanikiwa kuboresha na kupandisha hadhi Hospitali ya Mwananyamala kuwa Hospitali ya Mkoa, ikiwa pamoja na kujengwa Maabara ya kisasa, wodi mpya ya wazazi na watoto, na mengine mengi, na sasa matibabu yote yatakuwa yanapatika na pia madaktari bingwa watakuwepo hapo katika Hospital hiyo.

3-Pia alisema kuwa katika wakati wake alifanikiwa kuishawishi serikali kujenga shule na alifanikiwa kujenga shule tano katika Jimbo la Kinondoni chini ya uongozi wake uliopita kuanzia mwaka 2005 mpaka 2010, wakati kabla ya hapo kulikuwa na shule moja tu. pia alieleza kuwa suala la Walimu limeshashughulikiwa na kwa sasa Chuo kikuu cha Dodoma kitakuwa kina chukua wanafunzi takriban elfu tano ambao wanasomea uwalimu tu. kwa hiyo nimategemeo yake kuwa Vijana wengi watajitokeza ili kuchukua nafasi hizo kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu la leo na kesho.

Mwisho aliwaomba wananchi wa mpe kura za ndio Mh: Jakaya Mrisho Kikwete katika nafasi ya Urais, Diwani wa kata hiyo Mzee Chilu Manga na yeye Mweneyewe katika nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kinondoni.
Diwani wa kata ya Tandale Ndugu Chilu Manga akimwaga sera zake kwa Wananchi wa kata hiyo wakati wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi zikifanyika katika Uwanja wa Mkunguje.
Diwani wa zamani wa kata hiyo ya Tandale Ndugu Mwilima akiwahutubia wananchi wa kata hiyo ya Tandale wakati wa kampeni za CCM zilizofanyika katika Uwanja wa Mkunguje.
Mh: Iddi Azzan Mgombea Ubunge Jimbo la kinondoni na Diwani wa kata ya Tandale Ndugu Chilu Manga wakiangalia wasanii waliokuwa wakiburudisha wakati wa kampeni hizo zilizofanyika Uwanja wa Mkunguje.
Mh: Iddi Azzan akimwambia kitu Diwani wa kata ya Tandale Ndugu Chilu manga. ikiwa Mwenyekiti wa kata hiyo ya Tandale anasikiliza kwa makini.
 Mh: Iddi Azzan akiwa anaangalia wasanii waliokuwa wa kiburudisha jukwaani   
Mh: Iddi Azzan akimuelekeza kitu Ndugu Macdonald huku mtoto mdogo akienda kukaa karibu yake akiwa ameshikilia picha ya Mgombea huyo. hii nikuonyesha jinsi gani anvokubalika kwa jamii.
Wananchi kata ya Tandale wakiwa wanamsikiza sera za Mgomba Ubunge Mh:Iddi Azzan na Mgombea Udiwani Ndugu Chilu Manga wakati wa kampeni zilizofanyika Uwanja wa Mkunguje.
Viongozi wa Jimbo la Kinondoni, Viongozi wa kata ya Tandale na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni wa pili kutoka kushoto Mh: Iddi Azzan  pamoja na Mgombea Udiwani kata ya Tandale wa tatu Kutoka kushoto Ndugu Chilu Manga wakiwa wamewasili katika uwanja wa kampeni wa Mkunguje uliopo kata ya Tandale.
Wananchi wakiwa wanashagilia kwa kuwasili kwa Viongozi hao katika uwanja wa kampeni wa Mkunguje uliopo kata ya Tandale.
Wasanii wa Mizengwe Kushoto na Fataki kulia wakitoa burudani katika uwanja wa kampeni wa Mkunguje kata ya Tandale Jimbo la Kinondoni.

    
Picha nne za hapo juu zikionyesha mapokezi ya Mgombea Ubunge  wa jimbo la kinondoni Mh: Iddi Azzan  katika Uwanja wa kampeni wa Mkunguje uliopo kata ya Tandale
WATOTO WA MKUBALI MH: IDDI AZZAN.
Mh: Iddi Azzan akishangilia na watoto wakati alipowasili nyumbani kwake baada ya kutoka kwanye kampeni zake zilizofanyika uwanja wa Mkunguje kata ya Tandale.