Wednesday, August 14, 2013

MUGABE AWAPIGA VIJEMBE WAPINZANI


Rais aliyechaguliwa tena kutawala kwa muhula mwingine nchini Zimbabwe Robert Mugabe, amewaambia wapinzani wake kwenye uchaguzi uliokamilika hivi karubini kuwa ikiwa hawajapendezwa na matokeo ya uchaguzi basi 'wajinyonge'.

Mugabe aliongeza kuwa hawezi kurudi kwenye serikali ya muungano iliyoafikiwa kutokana na vurugu zilizofuata uchaguzi mkuu wa mwaka 2008.Morgan Tsvangirai, anayeongoza chama cha upinzani MDC, alisusia sherehe hizo ambapo Mugabe alitoa hotuba yake ya kwanza tangu kushinda uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 31 mwezi Julai.Mugabe aliyatoa matamshi yake makali kwenye sherehe za kuadhimisha siku ya mashuja waliopigania uhuru wa Zimbabwe.

MDC kimewasilisha malalamiko yake mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu hali ambayo imesababisha kucheleweshwa kuapishwa kwa Mugabe. Alishinda uchaguzi huo kwa asilimia sitini ya kuza zote. Hata hivyo majaji wengi wanasemekana kumuunga mkono Mugabe kwa hivyo huenda kesi ya MDC ikatupiliwa mbali.

Chama cha Mugabe Zanu-PF kilishinda wingi wa viti vya bunge kikipata zaidi ya thuluthi mbili ikiwa ni viti 160 ya viti kati ya 210 vya bunge zima.Sherehe za kuadhimisha siku ya mashujaa Zimbabwe, ni sherehe za kujivunia kwa wazimbabwe wakati ambapo nchi hiyo ilijipatia uhuru wake miaka ya sabini.

Hii leo Mugabe ameitoa hotuba yake ya kwanza katika eneo la kumbukumbu la vita hivyo na ambako baadhi ya wapigania uhuru wamezikwa.Hotuba za Mugabe zinasifika zaidi kwa siasa zake kali za kizalendo, na ambazo zaidi hulenga mkoloni wake wa zamani Uingereza na pia anatarajiwa kujipiga kifua kufuatia ushindi wake mkubwa katika uchaguzi mkuu uliopita mwezi jana.

Chama cha MDC kinasusia sherehe hizo katika kile kinachosema ilikuwa wizi mkubwa wa kura uliofanywa na chama cha Zanu-PF, kwa hivyo sherehe hii bila shaka itazongwa na siasa.Mugabe bado hajaapishwa kwa muhula wake wa saba akitawala Zimbabwe, kwa sababu ya kesi ya MDC mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi huo.

MDC kilisema kina ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa wizi wa kura ulitokea na kwamba kulikuwa na visa vingine vilivyohujumu matokeo ya uchaguzi huo ikiwemo, rushwa , dhuluma na kuvurugwa kwa daftari la wapiga kura.

WATU 44 WAUWAWA KINYAMA


Takriban waumini 44 wameuawa kwa kupigwa risasi wakiwa msikitini Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, kwa mujibu wa maafisa wa jimbo la Borno. Mauaji hayo yalifanyika wakati wa maombi ya asubuhi Jumapili , ingawa taarifa zimejitokeza Jumatatu , kutokana na hitilafu ya mawasiliano kwani jimbo hilo liko chini ya sheria ya hali ya hatari.

Washambulizi wanasemekana kuwa wanachama wa kundi la wapiganaji la Boko Haram, ambalo liliwaua maelfu ya watu tangu mwaka 2009.Shambulizi lilifanyika katika mji wa Konduga, ulio umbali wa kilomita 35 kutoka mji mkuu wa jimbo hilo , Maiduguri.

Gazeti la Daily Post, liliripoti kuwa watu wengine 26 walikuwa wanatibiwa kwa majeraha waliyopata wakati wa shambulizi hilo hospitalini Maiduguri. Mwanachama wa kikundi cha vijana kinachotoa ulinzi kwa raia, aliambia shirika la habari la Associated Press, kuwa wapiganaji wao wannne waliuawa walipojaribu kutoa kilio cha kutaka usaidizi. Raia wengine kumi na wawili, waliuawa katika kijiji cha Ngom kinachopakana na Maiduguri.

Rais Goodluck Jonathan alitangaza sheria ya hali ya hatari katika majimbo matatu Kaskazini Mashariki mwa nchi mnamo mwezi Mei wakati wanajeshi walipofanya operesheni dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu.Boko Haram linapigania eneo la Kaskazini mwa nchi likitaka kujitawala kwa kutumia sheria za kiisilamu.  Mwandishi wa BBC mjini Lagos, anasema kuwa wakati kundi hilo limekuwa likishambulia makanisa, pia limekuwa likishambulia misikiti.

Habari za mashambulizi hayo zilijitokeza wakati kanda ya video ya kiongozi wa kundi hilo Abubakar Shekau, ilipotolewa akidai kundi hilo kuhusika na mashambulizi hayo ikiwemo kushambulizi dhidi ya vituo vya polisi na kambi za jeshi.

WAFUASI WA MORSI WATAWANYWA MISRI



Polisi nchini Misri, wametumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji wanaomuunga mkono rais aliyeondolewa mamlakani Mohammed Morsi wakati wa maandamano yao mjini Cairo.Vikosi vya usalama viliingilia maandamano hayo baada ya wafuasi wa Morsi kukabiliana na mahasimu wao wa kisiasa.

Morsi aliondolewa mamlakani na viongozi wa jeshi mwezi Julai kufuatia maandamano makubwa sana.Walioshuhudia vurugu hizo walirushiana mawe na chupa huku watoto na wanawake wakikimbilia usalama wao.Tangu hapo jeshi limeweka serikali ya mpito.

Wafuasi wa Morsi aliyeingia mamlakani baada ya vuguvugu la kiisilamu la Brotherhood kushinda uchaguzi wa rais, wanakataa kukubali serikali mpya ya mpito wakisisitiza kuwa lazima rais wao arejeshwe mamlakani. Vurugu za Jumanne zilianza wakati wafuasi wa Morsi, walipotembea hadi sehemu moja ya Cairo ambako watu wengi wanapinga vuguvugu la Muslim Brotherhood.

Waandamanaji hao walijaribu kuingia katika ofisi za wizara moja ingawa polisi waliwalazimisha kuondoka kwa nguvu.Wakaazi wa eneo hilo walianza kuwakejeli waandamanaji na hapo ndipo polisi walipoingilia mzozo huo.Mamilioni ya wamisri waliandamana kumtaka Morsi aondolewe mamlakani ingawa wadadisi wanasema kuwa kuondolewa kwake kunaonekana kuzorotesha migawanyiko ya kisiasa iliyoko kwa sasa.

Wafuasi wake wamekuwa wakipiga kambi mjini Cairo wakitaka arejeshwe mamlakani. Maafisa wa usalama walitishia kuondoa mahema waliyoweka wafuasi wa Morsi ambako wamekuwa wakipiga kambi lakini wakabatili uamuzi wao baada ya kuamua kuuakhirisha.

Monday, August 12, 2013

NEY ATAFUTWA

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Ney wa Mitego, ameweka wazi kuwa ikitokea amefariki dunia hatohitaji kamati kwa ajili ya kuendesha mipango ya msiba wake, kwa kile anachodai kuwa kamati hizo zipo kwa ajili ya kuvuna pesa.

Hayo aliweka wazi baada kupokea ujumbe mfupi kwenye simu yake wenye vitisho uliotokana na mashairi alioimba kwenye single yake mpya ya 'Salaam zao' .

Ujumbe huyo wa vitisho ambao umepokelewa na msanii huyo umekuja mara baada ya msanii huyo kuachia single yake hiyo ambapo mmoja ya mashahiri ni juu ya hela za rambirambi zilizopatikana katika msiba wa msanii Ngwear pamoja na Kanumba kushindwa kuwafikia walengwa.

Akizungumza na jarida la Maisha, mara baada ya kutuma ujumbe alioupokea wa vitisho kwenye ukurasa wake wa 'Instagram', Ney wa Mitego aliweka wazi kuwa amepokea ujumbe wa vitisho mara baada ya kuachia nyimbo hiyo.

Alisema kuwa amepokea ujumbe mbalimbali ambazo zipo zinazowataja wahusika moja kwa moja wale waliohusika kula rambirambi, huku wengine wakimtumia ujumbe wa kumtisha kwa kile alichokiimba katika nyimbo hiyo.

"Mimi hata ikitokea nakufa leo sihitaji mtu yeyote yule anaweka kamati ya mazishi yangu kwani najua kitakachotokea siyo mazishi bali ni kula hela na rambirambi hizo kushindwa kutimiza malengo kama yalivyokusudiwa" alisema Ney wa Mitego.

Aliongezea kuwa hawezi kuacha kuimba ukweli hata kama ataendelea kupokea vitisho, msanii huyo ameachia single yake mpya inayokwenda kwa jina la Salaam zao.

BAKWATA YATAKA UCHUNGUZI WA PONDA


Baraza la waisilamu Tanzania limeunga mkono kauli ya Jumuiya ya taasisi za kisilamu za kuitaka serikali kuchunguza kwa kina tukio lililopelekea kupigwa risasasi kwa mhubiri wa kiisilamu Sheikh Issa Ponda.

Taarifa imetolewa na kaimu mufti wa Tanzania Al Had Musa Salum. Pamoja ya kwamba (BAKWATA) limekuwa likipingana na misimamo ya Sheikh Ponda limesema serikali ilikuwa na nafasi ya kumkamata Ponda kwa kufuata mkondo wa sheria.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari zilizopatikana mjini Dar es Salaam, Baruan Muhuza, sheikh huyo ambaye amekuwa katika mivutano ya mara kwa mara na serikali ya nchi hiyo alipigwa risasi baada ya kutokea vurugu kwenye mkutano wa mawaidha ya baraza la sikukuu ya Idd el Fitr.

Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Alhajj Mussa Kundecha, amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam  kuwa endapo serikali haitachukua hatua itakayowaridhisha Waislamu, wataamua kufikiria upya mustakabali wao na serikali ya Tanzania.

Sheikh Ponda amelazwa katika hospitali ya taifa, Muhimbili, mjini Dar es Salaam akiuguza jeraha la risasi huku akiwa chini ya ulinzi wa askari kanzu.

Msemaji wa Jeshi la polisi, Advera Senso ameiambia alisema kuwa jeshi lake kwa kushirikiana na jukwaa la haki jinai wameunda kikosi kazi kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa tukio hilo huku akikana kuwa Sheikh Ponda alipigwa risasi na polisi.

Senso amewalaumu wafuasi wa Sheikh Ponda kwa kuwazuia askari kumkamata Sheikh huyo kwa kuwarushia mawe; hatua iliyosababisha askari hao kufyatua risasi hewani ili kuwatawanya na hata hivyo wafuasi hao walifanikiwa kumtorosha kiongozi huyo wa kidini.

Taarifa za jumuiya hiyo ambayo inajulikana zaidi Tanzania kama Shura ya Maimamu zinasema kuwa Sheikh Ponda ambaye polisi wanasema walikuwa wakimtafuta kwa tuhuma za kutoa matamko ya uchochezi, alisafirishwa usiku kutoka mji wa Morogoro hadi Dar es Salaam zaidi ya kilomita 200.

Sheikh Ponda kwa sasa anatumikia kifungo cha nje cha mwaka mmoja alichohukumiwa mapema mwaka huu baada ya kukutwa na makosa kadhaa ikiwemo uchochezi wa kuharibu mali za watu.

RAIS MUGABE AHUTUBIA KWA MARA YA KWANZA


Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anatarajiwa kutoa hotuba yake ya kwanza tangu kushinda uchaguzi mkuu wa Zimbabwe zaidi ya wiki moja iliyopita.Mugabe atahutubia umma wakati wa sherehe za kuadhimisha siku ya mashujaa mjini Harare kuwakumbuk wale waliofariki wakipigania uhuru wa taifa hilo.
Chama hicho kimewasilisha malalamiko yake kuhusu uchaguzi mkuu ambao kinasema ulikumbwa na wizi wa kura kikitaka uchaguzi huo kurejelewa.Chama pinzani cha MDC, chake waziri mkuu Morgan Tsvangirai, kitasusia sherehe hizo.

Bwana Mugabe alishinda 61% ya kura kwenye uchaguzi huo uliokamilika tarehe 31 mwezi Julai, huku mpinzani wake Morgan Tsvangirai akichukua nafasi ya pili kwa 35% ya kura zilizopigwa.

Chama cha Mugabe Zanu-PF kilishinda wingi wa viti vya bunge kikipata zaidi ya thuluthi mbili ikiwa ni viti 160 ya viti kati ya 210 vya bunge zima.

Sherehe za kuadhimisha siku ya mashujaa Zimbabwe, ni sherehe za kujivunia kwa wazimbabwe wakati ambapo nchi hiyo ilijipatia uhuru wake miaka ya sabini.

Hii leo Mugabe atatoa hotuba yake ya kwanza katika eneo la kumbukumbu la vita hivyo na ambako baadhi ya wapigania uhuru wamezikwa.

Hotuba za Mugabe zinasifika zaidi kwa siasa zake kali za kizalendo, na ambazo zaidi hulenga mkoloni wake wa zamani Uingereza na pia anatarajiwa kujipiga kifua kufuatia ushindi wake mkubwa katika uchaguzi mkuu uliopita mwezi jana.

Chama cha MDC kinasusia sherehe hizo katika kile kinachosema ilikuwa wizi mkubwa wa kura uliofanywa na chama cha Zanu-PF, kwa hivyo sherehe hii bila shaka itazongwa na siasa.
Mugabe bado hajaapishwa kwa muhula wake wa saba akitawala Zimbabwe, kwa sababu ya kesi ya MDC mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi huo.
MDC kilisema kina ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa wizi wa kura ulitokea na kwamba kulikuwa na visa vingine vilivyohujumu matokeo ya uchaguzi huo ikiwemo, rushwa , dhuluma na kuvurugwa kwa daftari la wapiga kura.

TNG YATAMBULISHA SINGLE YAO MPYA

 Kundi la TNG la muziki wa bongo fleva nchini wakijiandaa kupanda jukwaani kwa ajili ya kutambulisha nyimbo yao mpya iliyokwenda kwa jina la 'Crazy Love katika ukumbi wa Dar Live jijini Dar es Salaam siku ya Idi Mosi

 Msanii anayeunda kundi la TNG Chiwaman (kulia) akiwa sambamba na kiongozi wa kundi la Wanaume family pamoja na Rose Ndauka ambaye ameshirikishwa kwenye nyimbo ya Crazy Love ambayo ilitambulishwa usiku huo



Monday, August 5, 2013

WAFUASI WA MDC WADAI KUSHAMBULIWA ZIM



Siku moja baada ya Rais Robert Mugabe na Zanu PF kutangazwa kushinda uchaguzi Mkuu nchini humo, baadhi ya wafuasi wa upinzani kutoka chama cha MDC wanasema wameshambuliwa na wenzao wa ZANU PF.

Baadhi ya dola za Magharibi ikiwa ni pamoja na Marekani na Uingereza, zimetilia shaka iwapo uchaguzi huo ulifanyika kwa uwazi. adai hayo yanakuja siku moja baada ya matokeo rasmi ya uchaguzi uliofanyika Jumatano kutolewa na kumpa ushindi rais Robert Mugabe. Chama chake Zanu-PF kilipata thuluthi tatu ya viti vya bunge.

Watu 11 mjini Harare na wengine 20 kutoka mkoa wa Mashonaland, wanasema kuwa walishambuliwa na wafuasi wa Zanu-PF wanaojulikana sana baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa.

WATUHUMIWA WATESWA NA POLISI

Washtakiwa wanne wanaokabiliwa na kesi ya wizi wa kutumia silaha wameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kutokuwa na imani na afya zao kutokana na mateso waliyoyapata kwa polisi wa kituo cha Oysterbay wakati wa kuchukuliwa maelezo.

Washitakiwa hao ni Ally Hashimu, Donald Nzwenka, Michael Pascal, Kulwa Adamson na Yohanna, watuhumiwa hao walifikishwa mahakamani hapo wiki iliyopita na baada ya kusomewa makosa yao mawili yanayowakabili mbele ya wakili wa serikali Flora Massawe mbele ya Hakimu Aloyce Katemana

Walidai kwa Hakimu Katemana kuwa hawana imani na afya zao kwani walipigwa na polisi hao wakati wa kuchukuliwa maelezo na kulazimishwa kukubali makosa wasiyoyafanya na mmoja wa washtakiwa hao, alisema kuwa ameingizwa msumari sikioni hivyo hasikii vizuri pamoja na kumkata na panga kwenye ncha za vidole vya miguu.

SELENA GOMEZ AFICHUA SIRI YA BIEBER


Ripoti kwamba Selena Gomez na Justin Bieber wanarudiana na kuachana mara kwa mara zimepata ufumbuzi kutoka kwa kimwana huyo.

"Nimemfahamu Bieber kwa muda mrefu na tunafurahiana kampani ya kila mmoja wetu mara kwa mara " alisema Selena aliliambia Associated Press aliongezea kuwa " mimi niko single na ninafurahia hilo"

MAREKANI YAFUNGA BALOZI ZAKE AFRIKA KASKAZINI


Marekani imesema kuwa itafunga balozi zake kadhaa Kaskazini mwa Afrika na Mashariki ya kati hadi Jumamosi wiki ijayo kwa sababu ya hofu ya kushambuliwa na makundi ya wapiganaji wa kiisilamu.Balozi 21 za Marekani na ofisi zake zilifungwa Jumapili.

Uingereza ilisema kuwa Ubalozi wake nchini Yemen utasalia kufungwa hadi mwishoni kwa sherehe za siku kuu ya IDD siku ya Alhamisi na kufunguliwa siku ya Jumanne.Wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema kuwa kufungwa kwa balozi hizo ni kutokana na serikali kuchukua tahadhari kubwa na wala sio jibu lake kwa tisho jipya la mashambulizi.
Wakati huohuo, balozi za Marekani katika miji ya Algiers, Kabul na Baghdad ni miongoni mwa zile zitakazofungwa na kutarajiwa kufunguliwa Jumatatu wiki ijayo.

AUWAWA BAADA YA KUMNYONGA MKE WAKE

Mwanaume mmoja mkazi wa kijiji cha Kisangwa kata ya Mcharo wilaya ya Bunda mkoa wa Mara, Batule Masanja anadaiwa kumuua mkewa wake kwa kumnyonga shingo kwa kutumia mikono yake kisha na yeye kuuwawa na wananchi wenye hasira kali.

Tukio hilo lilithibitishwa na polisi wilayani hapo, lilitokea usiku wa kuamkia juzi katika kijiji cha Kisangwa kata ya Mcharo kwenye sherehe ya ufunguzi wa nyumba ya ndugu yao.

Friday, August 2, 2013

WASHUKIWA WA UGAIDI KULIPWA FIDIA KENYA



Mahakama nchini Kenya, imeamuru waathiriwa kumi na moja waliohamishwa kinyume na sheria kwa madai ya kuwa washukiwa wa ugaidi walipwe fidia, Walikuwa sehemu ya idadi kubwa zaidi ya washukiwa wa ugaidi waliohamishiswa nchi ya kigeni kinyume na sheria.

Mahakama kwa hivyo imeamuru serikali ya Kenya kuwalipa fidia ya kima cha dola 460,000 waathiriwa wa kitendo hicho.Washukiwa hao walikamatwa mwaka 2007 na kuhamishiwa hadi Somalia na wengine wakipelekwa Ethiopia ili kuhojiwa na mashirika ya kijasusi ikiwemo FBI na CIA.Waathiriwa hao walikuwa miongoni wa washukiwa zaidi ya 100 wa ugaidi waliozuiliwa nchini Ethiopia.

Waathiriwa hao wakiwemo wakenya wanane na raia wawili wa Tanzania pamoja na raia mmoja wa Rwanda, walikamatwa katika ufuo wa bahari nchini Kenya na maafisa wa usalama kabla ya kupelekwa kwa lazima nchini Somalia na hatimaye Ethiopia.

CWT YATOA TAMKO WALIMU KUFELI

RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, amesema matokeo mabaya ya walimu yaliyotangazwa na Baraza la Mtihani Tanzania (NECTA) hayashangazi kwani walishaiambia serikali iwe innapeleka vyuoni wanafunzi wenye ufaulu mzuri lakini haifanyi hivyo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mukoba alipozungumza na waandishi wa habari alisisitiza kuwa pamoja na kupigia kelele suala hilo, lakini serikali imekuwa ikiendelea kupeleka wanafunzi wabovu hivyo imevuna ilichopanda.

Alisema kuwa matokeo hayo pia yamechangiwa na serikali kutosikiliza madai yao kwani tangu mwaka jana walimu na serikali wamekuwa na ugomvi usiokuwa na majibu.

Aliongeza kuwa madai ambayo walikuwa wakiyadai ni pamoja na nyongeza ya asilimia 100 ya posho ya kufundishia, asilimia 50 ya mazingira magumu, lakini hadi sasa wamepewa nyongeza ya asilimia 8 tu ya nyongeza ya mshahara.

"Ukipanda ujinga unalima uzuzu, sio mara ya kwanza hali hii inatokea,Serikali imeendelea kuziba kwa suala nyeti kama hili la elimu huku ukitarajia taifa kwenda mbali" alisema Mukoba.

WANAFUNZI 30 WAJAZWA MIMBA ROMBO

Wanafunzi 30 kutoka shule mbalimbali za sekondari katika wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro walishindwa kuendelea na masomo katika kipindi cha mwaka 2012 kutokana na kupata ujauzito.

Wanafunzi hao ambao walikatisha masomo wengi wao wanaelezewa kuwa walikuwa kidato cha nne hivyo kujikuta wakitia doa ndoto zao kutokana na kutoendelea na masomo.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari ofisini kwake Ofisa Elimu wa sekondari katika wilaya ya Rombo, Juma Kinanda alisema kati ya wanafunzi hao 30 wanafunzi 28 ni kutoka shule za sekondari za serikali na wawili kutoka shule binafsi.

Kinanda alisema tatizo la mimba shuleni bado ni tatizo ambalo limekuwa likisababisha baadhi ya watoto wa kike kukatisha masomo, na hivyo kuishia kuishi maisha ya mitihani baada ya ndoto zao kuzimika.

Aidha aliweka wazi kuwa tatizo hilo limezidi kuwa kubwa na baadhi ya wazazi kutoshtushwa na hali hiyo na kuona ni jambo la kawaida huku wengine wakidiriki kukataa kutoa ushirikiano pindi watoto wanapobainika kupata ujauzito.