Tuesday, November 12, 2013

MKUU WA SHULE ABAMBWA AKIVUJISHA MAJIBU YA MTIHANI

MKUU wa Shule ya Sekondari ya Nkinto wilaya ya Mkalama, Monica Sebastian (30) na mwalimu wa kawaida wa shule hiyo, Agaloslo Otieno (32), wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kuvujisha matihani wa kidato cha nne unaoendelea kufanyika hivi sasa nchini kote.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo lilitokea juzi, saa tatu usiku, katika shule hiyo kata ya Mwangeza tarafa ya Kirumi wilayani humo.

Alisema kuwa Mwalimu Agaloslo akiwa anasimamia mtihani katika Shule ya Sekondari Mwangeza, alikuwa anaandika baadhi ya maswali ya Kiswahili na Civics kwenye simu yake ya kingajani na kumtumia Mwalimu Monica, akiwa shuleni kwake Nkinto.

Kamwela alisema baada ya Monica kupata maswali hayo, alikuwa anayatafutia majibu akiwa chooni na wanafunzi walikuwa wanamfuata huko huko chooni ili awapatie majibu hayo.

"Lengo lao ilikuwa ni kuwasaidia wanafunzi ili waweze kufanya vizuri katika mtihani wao wa kidato cha nne mwaka huu. Wanafunzi waliambiwa kuwa wawe wanadanganya kwamba wanaenda kujisadia chooni ili wakapatiwe majibu na mkuu wa shule," alisema kamanda huyo na kuongeza; "Uchunguzi wa awali wa polisi unaonyesha kuwa, uvunjishaji huo ulifanyika kwa nyakati tofauti kati ya Mkuu wa Shule Monica na Mwalimu Agaloslo akiwa anasimamia mtihani huo katika shule nyingine.
“Baada ya Mwalimu Monica kutumiwa maswali alikuwa anajificha chooni na wanafunzi kwa nyakati tofauti huomba ruhusa kwa wasimamizi kwenda chooni kwa nia ya kujisaidia, ambapo humkuta mwalimu huyo na kuwapa maelekezo ya namna ya kujibu maswali hayo," alisema.

Alisema baada ya polisi kupata taarifa ya siri kutoka kwa wasamaria wema, waliweka mtego shuleni Nkinto na kufanikiwa kumkamata Mwalimu Monica, huku simu yake ikiwa na baadhi ya maswali ya mtihani.

Alisema polisi inaendelea na upelelezi zaidi, na kwamba mara utakapomalizika, watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayowakabili.

Friday, November 8, 2013

HOTUBA YA RAIS KIKWETE JANA

Mheshimiwa Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu;
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri;
Mheshimiwa Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni;
Waheshimiwa Wabunge;
Mabibi na Mabwana;

Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kukubali ombi langu na kutenga muda wenu ili niweze kuzungumza na Wabunge wa Bunge lako Tukufu kuhusu masuala muhimu kwa uhai, ustawi na maendeleo ya nchi yetu na watu wake.
Mheshimiwa Spika;
Nimeambiwa kuwa taarifa ilipotolewa kuwa ninaomba kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wabunge, kumekuwepo na dhana mbalimbali. Wapo waliodhani kuwa nakuja kuzungumzia mchakato wa kuunda Katiba mpya na hasa matukio ya wiki chache zilizopita. Wapo waliodhani nakuja kuzungumzia “Operesheni Tokomeza”. Tena wapo waliokwenda mbali na kufikiria kuwa nakuja kuwakaripia Waheshimiwa Wabunge waliotoa maoni yao kuelezea kasoro zilizojitokeza katika utekelezaji wa Operesheni hii muhimu. Na wapo pia waliodhani ninakuja kuzungumzia ushiriki wa majeshi yetu ya Tanzania katika Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa nchini Kongo.

Wednesday, November 6, 2013

MFANYAKAZI TBC AUWAWA

Mfanyakazi wa Shirika la Utangazaji Nchini TBC, pichani,RAMADHAN GIZE ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaosaidiwa kuwa ni majambazi usiku wa kuamkia leo katika eneo la UBUNGO Maziwa Jijini DSM.


Tukio hilo limetokea baada ya watu hao kuvamia duka moja katika eneo hilo la UBUNGO MAZIWA kwa lengo la kupora, ambapo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la MWARAMI RAJABU amejeruhiwa kwa kupigwa risasi na watu hao wanaosaidiwa kuwa majambazi.

Tuesday, October 29, 2013

KINANA AZIMA MAPINDUZI



Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alilazimika kuzima mapinduzi yaliyokuwa yamepangwa kuwang’oa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana ya chama hicho (UVCCM), Sadifa Juma Khamis na makamu wake, Mboni Muhita.

Jana Kinana akifungua mkutano wa Baraza Kuu la jumuiya hiyo, aliweka bayana kuwa mkutano huo haukuwa kwa ajili ya “kuibomoa UVCCM, bali kuijenga”, kauli ambayo inatajwa kuwa iliwavunja nguvu wajumbe waliokuwa wamepanga kuanzisha harakati za kuwatoa madarakani viongozi hao.

Habari zaidi kutoka Dodoma zilisema kauli ya Kinana iliongeza nguvu harakati za kujinasua za Sadifa ambaye usiku wa kuamkia jana, alikesha akifanya vikao vya kuwaomba radhi wenyeviti wa UVCCM wa mikoa na baadaye wajumbe wote wa Baraza Kuu.

“Hatua hiyo nadhani imemsaidia sana maana wenzake ndani ya umoja huo hawaridhiki na jinsi mambo yanavyokwenda, pamoja na uongozi wake. Wanaona kama hakidhi standards (viwango) zao,” kilisema chanzo chetu kutoka ndani ya mkutano huo.

MWANAFUNZI AJIUA KUONDOKA NA AIBU

MWANAFUNZI wa Darasa la tano Katika Shule ya Msingi Kitanda katika halmashauri ya wilaya ya Tunduru aliyefahamika kwa jina la Faudhia Suleiman Ally Kawalula (14) amejinyonga hadi kufa kwa madai ya kuondokana na aibu ya tukio la Wizi.

Mashuhuda wa Tukio hilo walisema kuwa Mwanafunzi huyo alikutwa akiwa aejinyoga kwa kutumia kamba asubuhi ya kuamkia oktoba 27 mwaka huu nda ya chumba alicho kuwa akilala nyumbani kwao.

Wakizungumzia chanzo cha tukio hilo kwa masharti ya kutotajwa majina yao gazetini miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa kabla ya mwanafunzi huyo kuchukua maamuzi hayo alituhumiwa kuiba Tsh. 5000 kwa muuza duka jirani na nyumba yao .

Walisema baada ya tukio hilo ambalo lilidaiwa kufanyika kwa ustadi mkubwa na alipo guindulia tayali akuwa amekwisha nunua nguo za ndani, mafuta ya kupaka na sabuni vitu ambavyo muuza duka huyo alivitaka
apewe ili aviuze kwa ajili ya kufidia fedha yake hali ambayo ilimuweka binti huyo katika aibu na kumfanya achukue hatua hiyo.

Monday, October 28, 2013

VIONGOZI CHADEMA WAZIPIGA KAVUKAVU

Mkutano wa Baraza la Uongozi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini juzi uligeuka ukumbi wa ngumi, baada ya Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba kushushiwa kipigo.

Mwigamba alishushiwa kipigo hicho na baadhi ya viongozi wenzake wa chama kwa madai ya usaliti na tayari amesimamishwa uongozi kwa muda usiojulikana.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas jana alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo na viongozi hao wa Chadema kufikishana polisi.

Alikutwa na zahama hiyo mbele ya viongozi wakuu wa Chadema Taifa, Mwenyekiti, Freeman Mbowe na mwasisi wa chama hicho, Edwin Mtei katika Hoteli ya Coridal Spring.

Saturday, October 19, 2013

TLC KUZINDUA FILAMU

Kundi la TLC linatalajia kufanya uzinduzi ya filamu yao mpya inayojulikana kwa jina la CrazySexyCool.

TLC inatarajia kuizindua filamu hiyo wiki ijayo ambapo teyari wameshaanza kuonesha baadhi ya vipande vya filamu hiyo.

MECHI YA YANGA NA SIMBA ULINZI WAIMARISHWA

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama vimejipanga ipasavyo kuakikisha Ulinzi unakuwepo Uwanja wa Taifa  wakati wa mchezo wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam jana,Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Kamishina Suleiman Kova alisema  mchezo wa leo utakuwa na mvuto mkubwa kwa mashabiki wa Tanzania na wale wa nchi za Afrika Mashariki tutokana na hali hiyo jeshi la Polisi limejipanga kupambana na hali yoyote ya uvunjifu wa amani itakayo jitokeza katika mchezo huo.

"Tunaomba wananchi wasiwe na shaka yeyote ya kiusalama na pia watupe ushirikiano wa kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi kwa jambo lolote wanaloisi linaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani kwa kipindi chote watakapokuwa ndani ya uwanja au nje."alisema Kova.

Wednesday, October 16, 2013

WAZEE YANGA YAJITAMBA KUINGO'A SIMBA

WAZEE wa Club ya Yanga wametamba kuwafunga watani wao wa jadi Simba katika mechi yao ya kesho kutwa inayotarajiwa kuchezwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ambapo wamedai kuwa mnyama lazima afe.

Akizungumza kwa niaba ya wazee hao na Waandishi wa Habari Dar es Salaam Katibu wa Baraza la Wazee Ibrahim Akilimali alidai kuwa  timu hiyo ndiyo inaanza kucheza mchezo wao wa ligi rasmi huku wakijitapa kumuua mnyama kutokana na maandalizi yao ambapo kikosi cha Yanga kitapanda dimbani huku kukiwa hakuna majeruhi.

Friday, October 4, 2013

SERIKALI KUBORESHA ELIMU NCHINI

SERIKALI inatakiwa kuboresha kwanza maslahi ya walimu na vifaa mashuleni ili kupatikane na matokeo makubwa (Big Result Now)

Hayo alisema Mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika wakati akikabidhi madawati 120 yenye thamani ya shmilioni 12 katika shule zilizoko Kata ya Manzese ambao walikuwa na uhaba wa madawati na kusababisha wanafunzi kukaa chini .

Alisema kuwa walimu wamekuwa wakililia maslahi yao kila siku lakini serikali haiwasikilizi hivyo itasababisha matokeo mabya ya mitihani kila siku.

COKE STUDIO YAZINDULIWA AFRIKA

KIPINDI cha muziki kinachojulikana kwa jina la Coke  studio Afrika chazinduliwa rasmi jana huku kikiwa na lengo la kuuboresha muziki wa Afrika uwe wa kisasa na unaolenga vijana.

Akizungumza katika uzinduzi huo Meneja bidhaa wa Coca Cola Tanzania, Maurice Njowoka aliweka wazi kuwa studio hiyo inathamini nguvu ya muziki katika kuwaleta watu pamoja bila kujali jinsia, lugha, dini na nchi.

Alisema kuwa kipindi hicho cha runinga kinachojumuisha nchi za Afrika Mashariki, kati na Magharibi kitawahusisha wanamuziki wa miondoko ya aina tofauti tofauti kutoka sehemu mbalimbali ili kupata mchanyato wa kisasa wenye asili ya Afrika.

Tuesday, October 1, 2013

WANAWAKE WAANDAMANA

NCHI ya Nigeria inakumbwa na uhaba wa wanaume wanaohitaji kuoa hali iliyosababisha wanawake zaidi ya elfu nane kuandamana.

Lengo la maandamano yao ni kushinikiza serikali kuwasaidia waolewe kutokana na uhaba wa wanaume hao uliojitokeza nchini humo.

Maandamano hayo yaliyofanyika nchini humo yalikuwa na nia ya kutatua tatizo hilo ingawa haikuweka wazi ni njia gani zitakazotumika kutatua uhaba huo wa wanaume.

Wanawake wengi walijitokeza katika maandamano hayo ambapo jumla ya wanawake 5380 waliopewa talaka, 2200 wajane, 1200 yatima, na 80 wengine kwa ajili ya kutatua tatizo hilo.

Wanawake hao walidai kuwa hawana uwezo hata wa kununua chakula cha siku hali inayopelekea kuhitaji kuolewa ili waweze kupata msaada kutoka kwa wanaume hao.

MAHALI YA WANAWAKE INAONGEZA UKATILI

IMEELEZWA kuwa  ukatili dhidi ya wanawake  katika ndoa unatokana na  kigezo cha
kulipiwa mahali ambayo imekuwa ikigeuka  kuwa ni adhabu  na chanzo cha mateso.

Hali hiyo imebainika kuwa  haitoi usawa  ndani ya jamii  kwani  mwanaume anaonekana yupo  juu na mwanamke kuwa chini  kutokana na wanaume kuwaona wanawake ni  mali yao Hayo yalielezwa jana na mwezeshaji  Fortunata Makafu  wakati akizungumza kwenye mafunzo ya siku mbili wilayani Chamwino yaliyoandaliwa na Wowap kwa kushirikiana na shirika la Tunaweza na oxfam kwa viongozi mbalimbali wa kiserikali, dini, watmaalufu, polisi na watendaji wa kata na vijiji.

Kutokana na hali hiyo alisema kuwa shirika hilo limekuwa likitoa elimu kwa jamii ilkuepuka ukatili huo  na mafanikio mbalimbali yamenza kuzaa matunda.Alisema kuwa hivi sasa  kuna unafuu mkubwa  katika  kushughulikia  ukatili wkijinsia  kutokana na jeshi hilo  kuweka dawati la jinsia.

MTOTO WA MIAKA MIWILI AJIFUNGUA

MTOTO wa miaka miwili wa nchini China, amejifungua baada ya madktari kugundua kuwa anamimba isiyokuwa.

Mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Xiao Feng alijifungua kwa njia ya upasuaji mara baada ya madkati hao kugundua kuwa anaujauzito huo usiokuwa.

Xiao alipelekwa hospitali mara baada ya tumbo lake kuwa kubwa hali ambayo ilimsababishia matatizo ya upumuaji ndipo madktari walipoamua kumfanyia uchunguzi.

MSHITAKIWA AACHIWA HURU KWA FAINI YA 1000

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemlipisha faini ya Sh.1000 raia wa Kenya Joshua Mulundi baada ya kumtia hatiani katika kesi ya kuidanganya polisi kuhusika kumteka Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka iliyokuwa ikimkabili.

Shauri hilo jana lililetwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Aloyce Katemana, kwa ajili ya mshtakiwa huyo kusomewa maelezo ya awali ambapo baada ya kusomewa maelezo hayo na upande wa mashtaka, Mhindi alikiri kutenda kosa na mahakama kumpa adhabu hiyo au kifungo cha miezi sita gerezani.

Hakimu Katemana aliieleza Mahakama hiyo kuwa baada ya mshtakiwa kukiri maelezo yote ya kosa,inamtia hatiani na kumsomea hukumu pamoja na adhabu.

Akisoma hukumu hiyo,alisema amezingatia maelezo ya upande wa mashtaka na maelezo ya mshtakiwa alipokuwa akiililia mahakama na hivyo kumpa adhabu ya kulipa faini ya Sh.1000 au kwenda gerezani miezi sita.