Wednesday, October 27, 2010

KATA YA HANANASIF BABU KUBWA KWA MHE.IDDI AZZAN

Mhe.Iddi Azzan akihutubia umati wa Wananchi wa Kata ya Hananasif akiwaeleza sera zake ikiwa ni kuboresha makazi holela, barabara, maji na kusimamia sheria za watoto iliyotungwa mwaka (2009).  
 Mjumbe wa Halimashauri kuu Mzee Hanzuruni akimuombea duwa Mhe.Iddi Azzan.
Mhe.Iddi Azzan akiwa jukwaani akimwaga sera zake kwa Wananchi wa kata ya Hananasifu.
Mmoja wa makada wa CCM Kijana Macdonald akiwahamasisha Wananchi kukipigia kura chama cha Mapinduzi.
Mgeni rasmi Mzee Hanzuruni akigawa kadi ya Chama Cha Mapidunzi kwa Mwanachama mpya katika mkutano huo wa kampeni. 
Mhe.Iddi Azzan akiwasalimia Wananchi wa Kata ya Hananasifu baada ya kuwasili hapo.
Wananchi walivyo furika kata ya Hananasifu. 
Viongozi wachama walizungukwa kila kona....!
Mtu kibaoooo...! 
 Wasaniii wa Fataki wakiburudisha jukwaani
Nafasi kulikuwa hakuna.
Watoto wakigombania kuushika mkono wa Mhe.Iddi Azzan



Watu nyomiiiii

Tuesday, October 26, 2010

MHE.IDDI AZZAN ARUDI KATA YA NDUGUMBI KWA MARA YA PILI.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa Mhe.Nape akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni Mhe.Iddi Azzan katika mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Ndugumbi.

Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Kinondoni Mhe.Iddi Azzan akiwahutubia Wananchi wa Kata ya Ndugumbi wa kati wa mkutano wake wa kampeni.

 Mhe.Nape akimnadi Mgombea Udiwani wa kata ya Ndugumbi Ndugu Mgonja.
 Mjumbe wa Halmashauri kuu taifa Mhe.Nape akiwahutubia Wana ndugumbi katika mkutano wa kampeni.
 Mhe.Nonda akiwahutbia Wananchi wa kata ya Ndugumbi.
 Chipikizi Mohammed akitoa mashairi yake kwa Wananchi wa kata ya ndugumbi.
 Mhe.Iddi Azzan akipeana mikono na Mjumbe wa Halimashauri kuu Mhe.Nape baada ya kuwasili hapo mkutanoni.
Mhe.Nape na Mhe.Iddi Azzan wakionekaniwa kuvutiwa na wasanii waliokuwa wakiburudisha hapo uwanjani.


 Wasanii wa kucheza na nyoka wakiwa uwanjani kuonyesha mbwembwe zao.
 Wananchi wakiwa katika hali ya kuburudika
 Mmoja wa wasambazaji wa Maji yenye Chata la CCM. Ndugu Aisha akiwa uwanjani kusambaza maji hayo.
Wananchi wakimsindikiza Mhe.Iddi Azzan na Ndugu Mgonja katika ofisi ya kata baada ya kumaliza mkutano.

MHE.IDDI AZZAN AFUNGUWA SHINA LA NGUVU KAZI.

Mhe.Iddi Azzan akilifungua shina hili la Nguvu kazi lilopo kata ya Ndugumbi.
Mhe.Iddi Azzan akilifungua shina hilo kwa kuondoa kitambaa ambacho kili funikiwa shina hilo.
Mhe.Iddi Azzan akipandisha bendera baada ya kulifungua shina hilo la Nguvu Kazi.
 Shina likonekaniwa katika mtazamo wake baada ya kufunduliwa rasmi na Mhe.Iddi Azzan.

Mhe.Iddi Azzan akiwa anapewa maelezo mafupi kuhusu shina hilo.

Sunday, October 24, 2010

MHE.IDDI AZZAN NA SONGORO MNYONGE WANAWEZA, MWANANYAMALA.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni Mhe.Iddi Azzan akiwahutubia Wananchi wa Mwananyamala katika mkutano wake wa kamepeni uliofanyika katika viwanja vya galilaya. aliwataka Wananchi kukipa kura Chama Cha Mapinduzi ili kuwapatia Huduma zilizobora. akitoa mfano kwa sasa mpango unaoendelea kwa kila kata ni kuhakikisha inajengwa Zahanati ambayo itakuwa inatoa huduma za kiafya ili kurahisisha na kuipungumzia mzigo Hospitali ya Mwananyamal.
Pia aliwaeleza kuhusiana na Suala la Maji kuwa Serikali iko katika harakati za kuhakikisha wananchi wanapata maji ikiwa wanashirikiana na wataalamu kutoka nje ambao teyari wameshaanza kufanya kazi hizo ili kuhakikisha Watanzania wanaondokana na shida hiyo.
Mwisho aliwaomba Wananchi wa kata hiyo kumchagua Mhe.Jakaya kikwete katika nafasi ya Urais, Udiwani katika kata hiyo Ndugu Songoro Mnyonge na katika nafasi ya Ubunge wa Jimbo hilo la Kinondoni yeye mwenyewe Mhe.Iddi Azza.. "KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI"
Mhe.Iddi Azzan akimnadi Mgombea Udiwani wa kata ya Mwananyamala Ndugu Songoro Mnyonge ili aweze kushirikiana nae katika kazi za kiserekali.
Bizainab Mwinyi ajiengua katika Chama Cha Wananchi CUF baada ya kuzikubali sera za Chama cha Mapinduzi CCM, bibi huyo alirejesha kadi yake ya CUF kwa Mhe.Iddi Azzan wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Mwananyamala. 
Bizainabu akikabiziwa mingaro ya CCM.
Mhe.Iddi Azzan akimtambulisha Chipukizi Mohammed.
Ndugu Rashid Kimbanga akiburudisha Wananchi kwa nyimbo yake ya CCM.

 Mhe.Iddi Azzan na Ndugu Songoro wakiwa meza kuu wanaangalia Wasanii wanavo burudisha
 "Baraka ya nyumba watoto" Watoto waikubali CCM
Wananchi wakisikiliza Sera za Wagombea.









MHE.IDDI AZZAN AWATOA WASIWASI WAFANYA BIASHARA WA BWAWANI,KATA YA KIJITONYAMA

Mhe.Asha Baraka ambaye ni mjumbe wa Halmashauri kuu akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Kinondoni Mhe.Iddi Azza katika Mkutano wa kampeni uliofanyika katika Viwanja vya Bwawani kata ya kijitonyama.
Mhe.Iddi Azzan akihutubia Wananchi wa kata ya Kijitonyama katika Viwanja vya Bwawani, aliwatoa wasiwasi wafanyabiashara kwa kuwaambia serikali inawatambua na kwamba sehemu yao inashughulikiwa na itakapo malizika watakabidhiwa wenyewe, alisema atasimamia imara sehemu hiyo ilikuhakikisha walewote wanaostahiki ndio wanapewa kipaumbele.
Mwisho aliwaomba wananchi hao wahakikishe wanakipigia kura Chama Cha Mapinduzi ili kupata Viongozi bora wanaojali maslahi ya Umma. kuanzia Urais,Ubunge na Udiwani.
Katibu wa wilaya ya Kinondoni akimnadi Mgombea Udiwani wa kata ya Kijitonyama Ndugu Bulembo kwenye uwanja wa kampeni wa Bwawani.
Mgombea Udiwani kata ya Kijitonyama Ndugu Bulembo akiomba ridhaa kwa Wananchi wa kata hiyo Kumchagua yeye awe diwani, pamoja na  Mbunge na Rais wote kutoka CCM ifikapo tarehe 31/10/2010 .
Ndugu Omari Kimbau ambaye ni diwani anaemaliza muda wake katika kata hiyo ya Kijitonyama akiwaomba     Wananchi wakichague Chama Cha Mapinduzi CCM.
Ndugu Nyakia ambaye ni Mwanafunzi wa Chuo kikuu akiwatoa hofu Wananchi na WanaCCM kwa kuwaambia kuwa  CCM ina wanachama wengi sana Vyuoni ambao wamejipanga imara kuhakikisha CCM inarudi madarakani.
Katibu wa Wilaya akigawa kadi kwa Wanachama wapya wapatao kumi katika Uwanja wa kampeni wa Bwawani uliopo kata ya Kijitonyama.
Wanachama wapya wakila kiapo cha kukikubali na Kukilinda Chama Cha Mapinduzi, katika uwanja wa Kampeni wa kata ya kijitonyama
Mhe.Iddi Azzan akiwa kwenye tabasamu kubwa.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni Mhe.Iddi Azzan akipigamakofi baada ya kuvutiwa na wasani waliokuwa wakiburudisha hapo.
Nyakia Mwanafunzi wa Chuo kikuu akiwa nyuma ya meza kuu pamoja na Viongozi na makada wa CCM.
Chipukizi Mohammed akitoa ujumbe kwa Wananchi wa Kata ya Kijitonyama katika Viwanja vya Bwawani.
Wananchi na Wana CCM walikuwa wengi kusililiza Sera za Wagombea.
Wananchi wakisikiliza sera za Chama Cha Mapinduzi.
Biashara kwa ajili ya kukisaidia Chama cha CCM.
Mzee wa mipango Mng'ombe kushoto pichani akiwa na Hassan na binti ambaye ni mwanacham wa chama cha CCM. wakiwa wanajadili kitu.
Timu ya mipango ya Ushindi ikiwa imetulia Juu ya Gari wakiangalia Utaratibu unavoendelea.
Wasanii wanao chipukia wakiburudisha jukwaani.
Wasanii wachanga wakiwa wanatumbuiza kwenye uwanja wa kampeni.
Mhe.Iddi Azzan akiwaaga Wananchi kwa kuwapatia mkono baada ya kumaliza mkutano wake wa kampeni.
Watoto waki sukumana ili wapate kumsalimia Mhe.Iddi Azzan.
Mhe.Iddi Azzan akisalimiana na watoto baada ya kumaliza mkutano wake wa kampeni.
Mhe.Iddi Azzan akiwa Ofisi ya kata ya Kijitonyama kwa ajili ya kutia saini kabla ya kuelekea kwenye mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika kata hiyo.
Mhe.Iddi Azzan akitoka katika ofisi ya kata baada ya kutia saini ya kuwasili katika kata hiyo.

Mhe.Iddi Azzan na Ndugu Bulembo wakielekea kwenye mkutano baada ya kutoka kwenye ofisi ya kata hiyo ya kijitonyama.