Showing posts with label Spots. Show all posts
Showing posts with label Spots. Show all posts

Friday, September 27, 2013

NGASSA KUWALIPA SIMBA MWENYEWE


Mshambuliaji wa Yanga na timu ya Taifa (Taifa Stars), Mrisho Ngassa ameamua kulipa mwenyewe deni lake la Sh45 milioni anazotakiwa kuilipa klabu ya Simba baada ya kuhukumiwa na Shirikisho la Soka nchini (TFF).

Awali Ngassa alikuwa ameweka ‘ngumu’ kulipa fedha hizo na kuzua tafrani kwa mashabiki na wanachama wa Yanga kuhusiana na adhabu yake ya kulipa fidia iliyotolewa na Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi ya Wachezaji ya TFF.

Kamati hiyo ilimfungia Ngassa kucheza mechi sita, adhabu ambayo amekwisha itumikia na kilichobakia sasa ni kulipa fedha hizo ili aweze kucheza mechi za Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Friday, July 12, 2013

YALIYOJILI MECHI YA TAMASHA LA MATUMAINI

 Baadhi ya wabunge wa timu ya Yanga wakifanya mazoezi kabla ya mechi iliyochezwa hivi karibuni uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam siku ya Tamasha la Matumaini
 Baadhi ya timu ya wabunge wa Simba na Yanga wakiingia uwanjani hapo kwa ajili ya mechi hiyo ambapo timu ya Yanga iliweza kuchukua kombe la ushindi kwa goli la penati