Wednesday, July 17, 2013

ANYIMWA DHAMANA KWA KOSA LA KUMBAKA MKEWE

Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Entebbe nchini Uganda imemnyima dhamana Charles Atayo(33) anayetuhumiwa kumbaka mke wake.

Atayo mkazi wa kijiji cha Nakigalala kilichoko mkoa wa Sisa, wilaya ya Wakiso aliamriwa kurudi katika gereza la kigo baada ya kukataliwa dhamana yake.

Mtuhumiwa huyu anadaiwa kumlazimisha mkewe ambaye hakutajwa jina kufanya naye mapenzi kwa lazima jambo lililotafsiriwa sawa na ubakaji

Katika utetezi wake Atayo alikanusha kumbaka mkewe kwa kuwa walifunga ndoa halali tangu mwka 2000 na kuzaa naye watoto watatu.

Katiba ya Uganda inasema kuwa mtu yeyote yule atakayemlazimisha mwingine kufanya naye mapenzi bila ridhaa yake ni sawa na ubakaji

HALI MBAYA ASKARI MWINGINE JWTZ

Askari mmoja wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kati ya 14 waliojeruhuwa katika shambulio la waasi hivi karibuni mjini Darfur, Sudan imezidi kuwa mbaya hivyo kulazimika kukimbizwa Khartoum kwa ajili ya matibabu zaidi.

Msemaji wa JWTZ , Kanali Kapambe Mgawe aliyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari ofisini kwake, alisema askari hao wako Darfur nchini Sudan huku 4 wakiwa chini ya uangalizi maalumu na 9 kupata nafuu huku wakingoja kukamilika kwa Uchunguzi wa Umoja wa Mataifa (UN) ili taeatibu za kuwaleta nyumbani zifanyike.

Kanali Mgawe alisema wanawasiliana na UN mara kwa mara na kuwa miili hiyo itatua nchini kwa kipindi cha hivi karibuni mara baada ya kukamilika kwa taratibu za Umoja wa Mataifa.

Monday, July 15, 2013

KUNDI LA 'TNG' LAJA KIVINGINE, WAMSHIRIKISHA ROSE NDAUKA KWENYE 'SINGLE' YAO MPYA


HATIMAYE msanii wa filamu nchini Rose Ndauka ameamua kuugeukia muziki wa kizazi kipya kwa kuingiza sauti kwenye nyimbo aliyoshirikishwa inayojulikana kwa jina la 'Crazy Man'.

Rose ameshirikishwa 'single' hiyo na kundi linalojulikana kwa jina la TNG, baada prodyuza wa muziki huo  Paul Matthysse  'P- Funk Majani', kubaini kipaji chake hicho kwenye upande wa kuimba.

Kundi hilo limeundwa na wasanii wawili akiwemo Agustino John 'Latino Man' pamoja na Maliki Bandawe ambaye anamahusiano ya kimapenzi na Rose Ndauka.

JUSTINE BIEBER AMUOMBA MSAMAHA BILL CLINTON MSAMAHA


Baada ya muimbaji nyota wa muziki wa Pop Justine Bieber kuripotiwa kukojoa katika ndoa kwenye mgahawa, muimbaji huyo ameamua kuomba msamaha kwa kitendo hicho alichokifanya

Muimbaji huyo, amempigia simu rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton kumuomba radhi kutokana na kumkashifu baada ya kuonekana katika video akijisaidia kwenye ndoo huku akimkashfu rais huyo.

Bieber alimpigia simu rais huyo kumuomba radhi kwa kumkashifu pamoja na kupulizia rangi picha za rais huyo katika jiko la mgahawa mmoja katika jiji la New York City mapema mwaka huu

PIGO TANZANIA, WANAJESHI 7 WAUWAA NA 14 KUJERUHIWA


Wanajeshi 7 kati ya 36 wameuwa Darfur, mauaji wa wanajeshi 7 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliokuwa wanalinda amani Darfur, Sudan wauwaa baada ya kushambuliwa na waasi wa Sudani.

Mbali na vifo hivyo askari wengine 14 wamejeruhiwa vibaya katika shambulizi la kushtukiza lililofanyika na kundi la waasi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, msemaji wa jeshi hilo Kanali Kapambala Mgawe, alisema wanajeshi hao walivamiwa wakati wakiwa kwenye msafara wa kuwasindikiza waangalizi wa amani ambao walikuwa wanatoka eneo la Khor Abeche kwenda Nyara Darfur.

Saturday, July 13, 2013

ABIRIA WA BODA BODA MJINI


Nyani amezoeleka kuonwa kwenye misitu lakini hii ni jambo la kushangaza kwa wapita njia baada ya dereva wa bodaboda kumpakiza nyani kama abiri 

ZAIDI YA WATANZANIA 250 WAKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA NJE YA NCHI


KAMISHINA wa tume ya kuratibu na kuthibiti madawa ya kulevya Christopher Shekiondo amebainisha kwamba watanzania wengi wanaokamatwa na dawa za kulevya nchi za nje adhabu zao mara nyingi zinakuwa kunyongwa au kifungo cha maisha jela.

Akizungumza kwa simu jana Kamishina huyo alisema, kwa kipindi cha muda wa mwaka mmoja anakumbuka zaidi ya watanzania zaidi ya 250 wamekamatwa katika nchi mbalimbali na dawa za kulevya.

Friday, July 12, 2013

MAANDAMANO ZAIDI KUFANYIKA MISRI LEO


Wafuasi na wapinzani wa rais wa Misri aliyeondolewa madarakani Mohamed Morsi wanajiandaa kwa maandamano makubwa mjini Cairo, huku waumini wa dini ya Kiislamu wakiadhimisha Ijumaa ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadan.

Wafuasi wa Bwana Morsi wanatarajia kuwa mamilioni ya raia wa nchi hiyo, wataendelea kuunga mkono wito wao wa kutaka Bwana Morsi kurejeshwa madarakani.

Wapinzani wa rais huyo wa zamani ambao waliandamana hadi rais huyo akaondolewa madarakani na jeshi watakusanyika katika medani ya Tahrir.

Watu kadhaa wameuawa kwenye ghasia zilizotokea tangu Morsi alipoondolewa.

Mwandishi wa BBC mjini Cairo, Jim Muir anasema vuguvugu la Muslim Brotherhood huenda liliwatenga raia wengi wakati wa utawala wa Morsi, lakini bado raia wengi wa nchi hiyo hawataki jeshi kuingilia masuala ya siasa.Marekani kutuma ndege za kivita Misri

Siku ya Alhamisi serikali ya Marekani, ilitoa wito kwa utawala mpya wa Misri, kusitisha harakati zake za kuwakamata wanachama wa vuguvugu la Muslim Brotherhood na kuonya dhidi ya kulenga kundi lolote.

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon vile vile ameonya utawala huo wa Misri kutotenga chama chochote cha kisiasa katika harakati za kutatua mzozo wa kisiasa unaokumba taifa hilo.

Hata hivyo msemaji wa Ikulu ya White House, Jay Carney amesema, utawala wa Washington hauamini kuwa ni lazima isitishe misaada yake ya Misri.

Marekani inatarajiwa kupeleka ndege nne za kivita aina ya F-16 nchini Misri, lakini haijathibitisha kuwa msaada huo utatolewa lini.

Serikali ya Marekani imesema, inachunguza ikiwa aumuzi huo wa jeshi la Misri kumuondoa madarakani rais Morsi ni mapinduzi ya Kijeshi kwa kuwa sheria za Marekani inazuia serikali kutoa misaada kwa nchi yoyote ambayo kiongozi aliyechaguliwa kwa njia ya kidemokrasia ataondolewa kupitia mapinduzi.

Wafuasi wa rais Morsi wamekuwa wakiandamana wiki nzima karibu na kambi ya kijeshi iliyoko Mashariki mwa mji mkuu wa Cairo, ambako wanaamini kuwa kiongozi wao anazuiliwa na maafisa wa kijeshi tangu alipoondolewa madarakani.

YALIYOJILI SIKU YA MATUMAINI

 Muimbaji Flora Mbasha akitumbuiza uwanja wa taifa siku ya Matumaini
 Kipa wa timu ya Simba mbunge Iddz Azzan akiingia uwanjani
 Baadhi ya wachezaji wa timu ya Bongo Movi akiwemo Ray wakijiandaa kuingia uwanjani

YALIYOJILI MECHI YA TAMASHA LA MATUMAINI

 Baadhi ya wabunge wa timu ya Yanga wakifanya mazoezi kabla ya mechi iliyochezwa hivi karibuni uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam siku ya Tamasha la Matumaini
 Baadhi ya timu ya wabunge wa Simba na Yanga wakiingia uwanjani hapo kwa ajili ya mechi hiyo ambapo timu ya Yanga iliweza kuchukua kombe la ushindi kwa goli la penati

Friday, August 5, 2011

Wabunge wa Dar ni noma katika ufuatiliaji.


Mh.Iddi Azzan Mbunge wa Jimbo la Kinondoni na Mh Azzan Zungu wakijaribu kupitia nyaraka.

Sunday, May 22, 2011

MH. IDDI AZZAN AKABIZI MEZA YA SHULE SECONDARI YA KAMBANGWA KINONDONI.

 Mh. Idd Azzan akiongea na wanafunzi kabla hajakabidhi meza hiyo.
MBUNGE wa Jimbo la Kinondoni (CCM) Idd Azzan, amekabidhi msaada wa meza ya maabara katika Shule ya Sekondari Kambangwa iliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam ikiwa ni moja ya ahadi zake alizotoa katika shule hiyo.
Akiongea kabla hajaenda kukabidhi meza hiyo, mbunge huyo alisema kwa muda mrefu alisikia kilio cha wanafunzi wa shule hiyo kuhusu vifaa vya maabara hivyo kwa kuanzia tu ametoa meza yenye vifaa vya maabara yenye thamani ya shilingi milioni 5,950,000/=.
    Naye mkuu wa shule hiyo, Bi Gaudencia Kimario, alimshukuru Azzan kwa msaada wake huo na kumwomba ashughulikie swala la hati ya jengo, umeme na komputer ambapo alikubali ombi hilo na kuahidi kulishughulikia mara moja.   
    Wanafunzi wa kikundi cha ngoma wakitoa burudani.
    Wanafunzi wakimsikiliza Mheshimiwa. 
     Mheshimiwa Iddi Azzan akizindua rasmi meza hiyo
    Baadhi ya wanafunzi wakiwa wameketi katika meza hiyo kwa kuonyesha utumikaje wake.
    Mwalimu mkuu, Gaudencia Kimario, akikabidhi zawadi kwa Mh. Azzan.

    Monday, February 14, 2011

    VIONGOZI WA NCHI WAKIOMBA DUWA KATIKA KIFO CHA DEREVA WA IKULU...!

     Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamo wake Mhe.Mohammed Gharib Bilal na Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Ndugu Rashid Othmani Kushoto kwenye picha wakisoma Dua ya pamoja kwa ajili ya Mwili wa Marehe Ramadhani Said Mkoma aliyefariki dunia kwa ajali ya gari iliyotokea Ruvu kwenye msafara wa Mama Salma.
    Makamu wa Rais Mhe.Mohammed Gharib Bilali akitoa salamu za pole kwa Wafiwa wa Marehemu.

    MANDHARI YA BUNGE.

    Hivi ndivyo mandhari ya bunge la Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania lilivyo huko dodoma, Waheshimiwa Wabunge wakiwa wamekaa kwa utulivu katika viti vyao wakisikiliza Maswali na Majibu, kutoka kwa Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge.

    Monday, January 24, 2011

    MHE.IDDI AZZAN MGENI RASMI KATIKA MCHEZO WA KIRAFIKI DHIDI YA WASHIRIKI MISS UTALII 2010/2011

    Mbunge wa Kinondoni Mhe. Idd Azzan akisalimiana na washiriki wa Miss Utalii Tanzania Kaskazini wakati wa Mchezo wa Kirafiki Dhidi ya warembo wa Mashariki.
    Washiriki Miss Utalii Tanzania- Kusini na Magharini kabla ya mchezo wao wa mpira wa miguu.
    washiriki Miss Utalii Tanzania 2010/2011
    wakila tizi katika Ufukwe wa Coco Beach jijini Dar.
    Washiriki Miss Utalii wakicheza mechi yao wenyewe kwa wenyewe.