Tuesday, October 1, 2013

MAHALI YA WANAWAKE INAONGEZA UKATILI

IMEELEZWA kuwa  ukatili dhidi ya wanawake  katika ndoa unatokana na  kigezo cha
kulipiwa mahali ambayo imekuwa ikigeuka  kuwa ni adhabu  na chanzo cha mateso.

Hali hiyo imebainika kuwa  haitoi usawa  ndani ya jamii  kwani  mwanaume anaonekana yupo  juu na mwanamke kuwa chini  kutokana na wanaume kuwaona wanawake ni  mali yao Hayo yalielezwa jana na mwezeshaji  Fortunata Makafu  wakati akizungumza kwenye mafunzo ya siku mbili wilayani Chamwino yaliyoandaliwa na Wowap kwa kushirikiana na shirika la Tunaweza na oxfam kwa viongozi mbalimbali wa kiserikali, dini, watmaalufu, polisi na watendaji wa kata na vijiji.

Kutokana na hali hiyo alisema kuwa shirika hilo limekuwa likitoa elimu kwa jamii ilkuepuka ukatili huo  na mafanikio mbalimbali yamenza kuzaa matunda.Alisema kuwa hivi sasa  kuna unafuu mkubwa  katika  kushughulikia  ukatili wkijinsia  kutokana na jeshi hilo  kuweka dawati la jinsia.


Hata hivyo alisema kuwa  hivi sasa ukatilii unaoendelea  na hata kuenea zaidi ni ule  unaotokana na  mira na desturi ambapo kuna jamii bado inaona kuwa ni haki kuoa wake wengi na kuwatumikisha kama  vibarua wao wa kutafuta mali.Mwezeshaji huyo alisema kuwa kama jamii inatapata elimu na kuelewa madhara
yatokanayo na ukatili wa kijinsia basi kutakuwa kumesaidia wanawake wengi kuishi
maisha yenye sitaha ndani ya familia zao.

Vile vile alisema kuwa katika kutekeleza mradui huo  Tunaweza kwa Tanzania inalenga
kuwafikia watu milioni  16  na ujumbe mkubwa ukiwa ni  ukatili dhidi ya wabnawake
haukubaliki ambapo kwa mkoa wa Dodoma mradi huo unatekelezwa kwa wilaya za Chamwino,
Kongwa na Bahi.

No comments:

Post a Comment