Tuesday, October 1, 2013

WANAWAKE WAANDAMANA

NCHI ya Nigeria inakumbwa na uhaba wa wanaume wanaohitaji kuoa hali iliyosababisha wanawake zaidi ya elfu nane kuandamana.

Lengo la maandamano yao ni kushinikiza serikali kuwasaidia waolewe kutokana na uhaba wa wanaume hao uliojitokeza nchini humo.

Maandamano hayo yaliyofanyika nchini humo yalikuwa na nia ya kutatua tatizo hilo ingawa haikuweka wazi ni njia gani zitakazotumika kutatua uhaba huo wa wanaume.

Wanawake wengi walijitokeza katika maandamano hayo ambapo jumla ya wanawake 5380 waliopewa talaka, 2200 wajane, 1200 yatima, na 80 wengine kwa ajili ya kutatua tatizo hilo.

Wanawake hao walidai kuwa hawana uwezo hata wa kununua chakula cha siku hali inayopelekea kuhitaji kuolewa ili waweze kupata msaada kutoka kwa wanaume hao.

No comments:

Post a Comment