Wednesday, July 17, 2013

ANYIMWA DHAMANA KWA KOSA LA KUMBAKA MKEWE

Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Entebbe nchini Uganda imemnyima dhamana Charles Atayo(33) anayetuhumiwa kumbaka mke wake.

Atayo mkazi wa kijiji cha Nakigalala kilichoko mkoa wa Sisa, wilaya ya Wakiso aliamriwa kurudi katika gereza la kigo baada ya kukataliwa dhamana yake.

Mtuhumiwa huyu anadaiwa kumlazimisha mkewe ambaye hakutajwa jina kufanya naye mapenzi kwa lazima jambo lililotafsiriwa sawa na ubakaji

Katika utetezi wake Atayo alikanusha kumbaka mkewe kwa kuwa walifunga ndoa halali tangu mwka 2000 na kuzaa naye watoto watatu.

Katiba ya Uganda inasema kuwa mtu yeyote yule atakayemlazimisha mwingine kufanya naye mapenzi bila ridhaa yake ni sawa na ubakaji

No comments:

Post a Comment