Wednesday, July 17, 2013

HALI MBAYA ASKARI MWINGINE JWTZ

Askari mmoja wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kati ya 14 waliojeruhuwa katika shambulio la waasi hivi karibuni mjini Darfur, Sudan imezidi kuwa mbaya hivyo kulazimika kukimbizwa Khartoum kwa ajili ya matibabu zaidi.

Msemaji wa JWTZ , Kanali Kapambe Mgawe aliyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari ofisini kwake, alisema askari hao wako Darfur nchini Sudan huku 4 wakiwa chini ya uangalizi maalumu na 9 kupata nafuu huku wakingoja kukamilika kwa Uchunguzi wa Umoja wa Mataifa (UN) ili taeatibu za kuwaleta nyumbani zifanyike.

Kanali Mgawe alisema wanawasiliana na UN mara kwa mara na kuwa miili hiyo itatua nchini kwa kipindi cha hivi karibuni mara baada ya kukamilika kwa taratibu za Umoja wa Mataifa.

No comments:

Post a Comment