Wednesday, July 17, 2013

BAADHI YA MADEREVA WA MALORI WANACHANGIA MAAMBUKIZI YA UKIMWI

Imeelezwa kuwa uchukuzi wa bidhaa kutumia malori kunachangia kuenea kwa maambukizi ya virusi vya Ukimwi nchini.

Kauli hiyo imetolewa na katibu wa taasisi isiyo ya kiserikali ya kupambana na matumizi mabaya ya mali za umma, Andekisye Mwakabalula.

Alisema mara kadhaa madereva hao wamekuwa wakitoa kisingizio cha kuharibikiwa magari kwa waajiri wao waweze kupata muda wa kufanya ngono

Alisema baadhi ya madereva wa malori wamekuwa na familia kubwa katika maeneo mbalimbali wanayoweka kambi hali inayowaweka hatarini kupata maambukizi ya UKIMWI.

Alisema licha ya kuwa na kisingizio cha ugumu wa maisha lakini wanawake hao wamekuwa wakiwakubalia kwa urahisi madereva hao wazae nao wakiamini wana uwezo mkubwa wa fedha

No comments:

Post a Comment