Tuesday, July 23, 2013

WIZI WATIKISA BENKI AFRIKA

Utafiti umegundua kuwa benki zilizopo kwenye ukanda wa nchi za Afrika Mashariki zinapoteza wastani wa sh. bilioni 80 kila mwaka kutokana na wizi wa mitandao.

Utafiti uliofanywa na kampuni ya Deloitte mwaka 2012 unaonyesha kuwa benki za kibiashara kwenye nchi za Afika Mashariki zinapoteza takriban zaid ya sh 80 bilioni

Hayo yalibainishwa na Rais wa Taasisi huru ya kimataifa isiyokuwa ya kiserikali inayohusika na kusimamia na kutoa mafunzo na maarifa ya mifumo ya mitandao (ISACA), Boniface Kanemba wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Kanemba  alisema kuwa wizi wa mtandao umekuwa ukifanyika sana katika benki na taasisi mbalimbali zisizokuwa za serikali ambapo kiasi hicho cha fedha huwa zinaibiwa kila mwaka.

No comments:

Post a Comment