Friday, August 2, 2013

CWT YATOA TAMKO WALIMU KUFELI

RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, amesema matokeo mabaya ya walimu yaliyotangazwa na Baraza la Mtihani Tanzania (NECTA) hayashangazi kwani walishaiambia serikali iwe innapeleka vyuoni wanafunzi wenye ufaulu mzuri lakini haifanyi hivyo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mukoba alipozungumza na waandishi wa habari alisisitiza kuwa pamoja na kupigia kelele suala hilo, lakini serikali imekuwa ikiendelea kupeleka wanafunzi wabovu hivyo imevuna ilichopanda.

Alisema kuwa matokeo hayo pia yamechangiwa na serikali kutosikiliza madai yao kwani tangu mwaka jana walimu na serikali wamekuwa na ugomvi usiokuwa na majibu.

Aliongeza kuwa madai ambayo walikuwa wakiyadai ni pamoja na nyongeza ya asilimia 100 ya posho ya kufundishia, asilimia 50 ya mazingira magumu, lakini hadi sasa wamepewa nyongeza ya asilimia 8 tu ya nyongeza ya mshahara.

"Ukipanda ujinga unalima uzuzu, sio mara ya kwanza hali hii inatokea,Serikali imeendelea kuziba kwa suala nyeti kama hili la elimu huku ukitarajia taifa kwenda mbali" alisema Mukoba.

No comments:

Post a Comment