Tuesday, August 20, 2013

MWANAMKE MWENYE NYWELE NDEFU DUNIANI


MWANAMKE anayetambulika kwa jina la Asha Mandela anaongoza kwa kuwa na rasta ndefu zaidi duniani zenye urefu wa futi 55.

Mwanamke huyo ambaye anadaiwa kuonywa na madakati juu ya urefu wa nywele zake unaweza kumsababishia tatizo la kupooza Asha amedai hawezi kuzikata nywele hizo.

Mama huyo aishiye Atlanta mwenye umri wa miaka 47 anayeweka rekodi ya kuwa na rasta ndefu duniani ameweka wazi humchukua siku mbili kuosha pamoja na kuzikausha nywele zake.

Katika moja ya mahojiano aliyowahi kufanya mwanamke huyo ameeleza kuwa nywele zake zimekuwa ni sehemu ya maisha yake na hatoweza kuzikata kwani akifanya hivyo ni sawa na kujiuua.

No comments:

Post a Comment