Friday, August 2, 2013

WANAFUNZI 30 WAJAZWA MIMBA ROMBO

Wanafunzi 30 kutoka shule mbalimbali za sekondari katika wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro walishindwa kuendelea na masomo katika kipindi cha mwaka 2012 kutokana na kupata ujauzito.

Wanafunzi hao ambao walikatisha masomo wengi wao wanaelezewa kuwa walikuwa kidato cha nne hivyo kujikuta wakitia doa ndoto zao kutokana na kutoendelea na masomo.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari ofisini kwake Ofisa Elimu wa sekondari katika wilaya ya Rombo, Juma Kinanda alisema kati ya wanafunzi hao 30 wanafunzi 28 ni kutoka shule za sekondari za serikali na wawili kutoka shule binafsi.

Kinanda alisema tatizo la mimba shuleni bado ni tatizo ambalo limekuwa likisababisha baadhi ya watoto wa kike kukatisha masomo, na hivyo kuishia kuishi maisha ya mitihani baada ya ndoto zao kuzimika.

Aidha aliweka wazi kuwa tatizo hilo limezidi kuwa kubwa na baadhi ya wazazi kutoshtushwa na hali hiyo na kuona ni jambo la kawaida huku wengine wakidiriki kukataa kutoa ushirikiano pindi watoto wanapobainika kupata ujauzito.

No comments:

Post a Comment