Wednesday, September 4, 2013

BINTI AMEZA SIMU

WIVU wa kimapenzi umemuweka matatani msichana anayeishi nchini Brazil, Adriana Andrade baada ya kuamua kumeza simu yake ya mkononi ili kumzuia mpenzi wake asisome 'message' katika simu yake.

Msichana huyo mwenye umri wa miaka 19 amejikuta akilazimika kuumeza simu hiyo baada ya kugundua alikuwa na message za ajabu ambazo zingezua utata pindi mpenzi wake angezisoma.

Habari zilizoripotiwa na mtandao wa Hispania Yipeta zilieleza kuwa msichana huyo aliamua kumeza simu yake ya mkononi baada ya mpenzi wake kutaka kusoma message zilizomo katika simu hiyo.

Mtandao huo uliendelea kuripoti kuwa baada ya tukio hilo msichana huyo alilazimika kufanyiwa upasuaji ili kutolewa simu hiyo tumboni mwake.

No comments:

Post a Comment