Monday, September 16, 2013

YANGA YAWASILISHA RUFAA YAKE

Klabu ya Yanga tayari imewasilisha rufaa yake kwa shirikisho la soka nchini TFF juu ya kucheza mchezo wake katika hali isiyokuwa na usalama na kuomba mchezo huo urudiwe katika uwanja wa ugenini kwa timu zote.

Mchezo hu ambao ulitawaliwa na vurugu kutoka kwa washabiki wa Mbeya City ulichezeshwa na mwamuzi Andrew Shamba kutoka mkoani Pwani ambaye pia hakutoka maamuzi sahihi kwa kukataa bao halali la mshambuliaji Didier Kavumbagu dakika ya 70 ya mchezo.Mashabiki wa Mbeya City walirusha chupa za bia na mawe kwenye bus la timu ya Yanga na kuvunja kioo cha bus kubwa upande wa dereva na kumjeruhi mkononi hali iliyoplekea wachezaji wa Yanga kucheza kwa hofu katika mchezo huo wakihofia usalama wao.

Afisa habari wa Yanga Baraka Kizuguto aliwasilisha taarifa hizo kwa kamisaa wa mchezo juu ya matukio hayo na ushahidi wa kipande cha chupa kilichorushwa na kumjeruhi dereva baada ya kupasua kioo.Tukio hilo la kabla ya mchezo lilipelekea timu ya Yanga kucheza kwa woga na wasiwasi juu ya usalama wao(under protest) kitu ambacho kikanuni kinairuhusu timu iliyokutwa na matatizo hayo kuka rufaa kuhusiana na hali ya usalama iliyojitokeza.

Aidha klabu ya Yanga pia inaomba kuhakikishwa usalama na shirikisho la soka nchini (TFF) katka mchezo wa siku ya jumatano dhidi ya timu ya Prisons vinginevyo inaomba mchezo huo pia uhamishiwe katika uwanja wa ugenini kutokana na kutokua na uhakika wa usalama.

Katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara ulimalizika kwa sare ya bao 1-1, mchezo uliofanyika katika dimba la uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

No comments:

Post a Comment