Friday, September 27, 2013

LUGHA YA MATUSI YAUPOTEZA MUZIKI WA MDUARA

Muimbaji wa bendi ya Njenje 'Wananjenje' John Kitime ameweka wazi sababu zinazopelekea muziki wa mduara kukosa soko na kushindwa kupata nafasi ya kupigwa kwenye vyombo vya habari.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii aliweka wazi kuwa sababu moja wapo ya nyimbo za mduara kukosa soko ni kutokana na maneno ya matusi yanayotumika katika nyimbo hizo.

Alisema baadhi ya wasanii waliowengi waliojiingiza katika muziki huo wamekuwa wakitumia lugha yenye maneno ya kificho 'matusi' hali inayopelekea kushindwa kupigwa katika redio mbalimbali nchini.

Alisema kuwa waimbaji wanaoibukia hivi sasa wanapoteza maana halisi ya muziki huo wa mduara hali inayopelekea muziki huo kukosa soko.

No comments:

Post a Comment