Sunday, September 1, 2013

WEMA SEPETU AMTOA MACHOZI MAMA KANUMBA


BAADA ya mama Kanumba Bi. Flora Mtegoa kutunzwa kitita cha sh. laki tano na msanii wa filamu nchini Wema Sepetu, kitendo hicho kilimtoa machozi mama huyo na kudai kuwa kila anapokutana na baadhi ya wasanii anajikuta kumkumbuka mtoto wake.

Kitendo hiko kilitokea mwishoni mwa wiki katika uzinduzi wa Filamu ya Elizabeth Michael iliyopewa jina la Foolish Age katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, ambapo mama Kanumba alijikuta akitokwa na machozi mfululizo mara baada ya kukutana na msanii huyo.

Mama huyo ambaye alijikuta akivutiwa na uchezaji wa Wema ukumbini hapo wakati bendi ya Machozi ikitumbuiza aliamua kumfuata na kutaka kumtunza kutokana na uchezaji wake.


Wema alishindwa kupokea hela hiyo aliyotunzwa na mama huyo na badala yake alianza kumtunza yeye hela hali ambayo ilimtoa machozi.

Wema alimpigia magoti mama huyo kwa ishara ya kuonyesha kuwa anamuheshimu, na kumpenda huku akizingatia alishawahi kuwa mama mkwe wake.

Akizungumza mara baada ya kutunza kitita cha fedha hizo mama huyo aliweka wazi kuwa kila anapokutana na wasanii ambao walikuwa wanaukalibi na mtoto wake huyo anajikuta anamkumbuka mwanaye.

No comments:

Post a Comment