Wednesday, September 25, 2013

MISS TANZANIA AGEUKIA FILAMU


HATIMAYE aliyekuwa Miss Tanzania 2011 Salha Israel ameamua kujitosa katika fani ya uigizaji ambapo teyari ameshaanza kuonekana kwenye moja ya filamu mpya iliyopo chini ya kampuni ya Ray, 'RJ'.

Salha ameonekana katika baadhi ya picha zilizotumwa kwenye mtandao wa Instagram zilizokuwa zikimuonesha akiwa 'location' akirekodi filamu hiyo ambayo amecheza kama mlinzi wa mtoto wa rais.

Akizungumza na jarida hii Jaqueline Massawe 'Wolper' ambaye amecheza kwenye movi hiyo kama mtoto wa rais aliweka wazi kuwa movi hiyo ilimuhitaji mtu anayefanana kama yeye ndiye maana chaguo la kwanza likamdondokea miss huyo.

Alisema kuwa Salha ameweza kuvaa huhusika katika movi hiyo na kuonesha uzoefu kucheza na kamera kama vile alishawahi kuigiza hapo mwanzo.

Salha amecheza kwenye filamu hiyo kama mlinzi wa mtoto wa rais, huku Wolper akicheza mtoto wa rais jina la filamu hiyo bado halijawekwa wazi na siku ya kutoka bado haijajulikana ingawa inasemekana kutoka hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment