Wednesday, September 4, 2013

MWANAMKE AMEZA HELA

Mwanamke wa kimarekani amelazwa hospitali baada ya kuumia kooni na tumboni wakati akijaribu kutoa kiasi kikubwa cha fedha alizozimeza kwa kutumia ufagio wa kusafisha choo.



Christie Black 43 mkazi wa Bulls Gap, katika jimbo la Tennessee, alipata majeraha hayo baada ya kushindwa kutoa dola za Marekani 5000 alizomuibia mpenzi wake ambaye ni Bobby Gulley.

Kwa mujibu wa taalifa ya polisi wa jimbo hilo, Christie, alichukua maamuzi hayo ili kukwepa kugawana fedha hizo na mpenzi wake huyo baada ya kutengana.

Taarifa hiyo iliweka wazi kuwa mara baada ya kujiingiza fagio hilo tumboni kupitia mdomoni, mwanamke huyo alisikia maumivu makali kutokana na michubuko iliyomfanya atokwe na damu mfululizo.

Hali ya mwanamke huyo inaendelea vizuri baada ya kuwahishwa hospitali alikopewa matibabu kwa haraka.

Taarifa hiyo ya polisi iliweka bayana kuwa walipata taarifa ya tukio hilo kutokana na mpenzi wake huyo aliyekwenda kushitaki kuibiwa fedha hizo na kwamba baada ya upelelezi ndipo walipombaini mwanamke huyo akiwa taabani.

Alipohojiwa mwanamke huyo juu ya uamuzi wa kumeza kiasi kikubwa cha fedha alisema alikuwa anataka zikamsaidia kujiendeleza kimaisha baada ya kupata taalifa kuwa mpenzi wake anapanga kumuacha.

No comments:

Post a Comment