Friday, September 20, 2013

IDD AZZAN AWAASA WAHITIMU DARASA LA SABA


MBUNGE wa Jimbo la Kinondoni Idd Azzan amewataka wanafunzi waliomaliza elimu ya darasa la saba wasijidumbukize katika makundi ya madawa ya kulevya na badala yake waendelee na masomo ili wapate mafanikio hapo baadaye.

Hayo alisema juzi katika mahafali ya pili ya darasa la saba katika shule ya msingi ya hekima iliyopo Tandale jijini Dar es Salaam.

Alisema kuna ushawishi mkubwa wa wanafunzi wanaomaliza darasa la saba kuingia katika vishawishi vya uvutaji wa madawa ya kulevya kwa sababu wanamuda mrefu wanakuwa nyumbani hivyo hujifunza vitu mbalimbali ambavyo vingine ni kujiingiza katika makundi yasiyofaa.

Hivyo aliwataka wazazi na walezi wawapeleke watoto wao shule hata kama hajabahatika kuchaguliwa kujiunga  kidato cha kwanza.


Vile vile, aliwataka wazazi hao wawapeleke  watoto wao pre form one huku wakiwa wanasubili majibu yao kutoka na si kumuacha nyumbani na kumsababishia kujiunga katika makundi maovu.

Pia katika mahafali hayo mwalimu mkuu wa  shule hiyo Munga Mtengeti alimwambia Mbunge huyo kuwa shule yao inaupungufu wa madawati 363 na vyumba vya madarasa 3 na hawana uzio katika shule hiyo hali inayosababisha kupata kero nyingi kutoka katika nyumba zilizokuwa karibu na shule hiyo.

Hata hivyo Mbunge huyo ameahidi kutoa madawati 100,ma kujenga chumba kimoja cha darasa na amewataka wazazi na walezi wa shule hiyo kujichangisha wenyewe kwa wenyewe kwa ajili  ya kujenga vyumba viwili vya madarasa.

Katika suala la uzio wa shule Azzan amewata uongozi mzima wa shule wakishrikiana na wazazi waanze kujenga uzio huo na watakapofikia yeye atamalizia ili kuondoa kero wanazopata wanafunzi hivi sasa.

No comments:

Post a Comment