Tuesday, October 5, 2010

kampeni ya saidia taifa stars ishinde yazinduliwa jana jijini dar

Mgeni rasmi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Muhammed Seif Khatib akibandika stika kwenye ramani ya Tanzania kuashiria kuwa kampeni kubwa ya kuhamasisha watanzania waweze kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu ya taifa katika mchezo wake muhimu dhidi ya timu ya timu ya Taifa ya Morocco hapo jumamosi,Oktoba 9 2010 imezinduliwa rasmi.kati ni Meneja Mkuu wa Uhusiano, mawasiliano na Jamii kutoka kampuni ya bia ya Serengeti Dada Teddy na Rais wa TFF, Leodga Tenga wakishuhudia tukio hilo mchana huu. 
Rais wa TFF,Leodga Tenga akitoa ufafanuzi kuhusiana na kiingilio cha mchezo huo utakaofanyika siku ya jumamosi,mbali ya hiyo Tenga amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo na kuwapa moyo wachezaji wa timu ya Taifa na hatimaye kushinda.

No comments:

Post a Comment