Monday, October 4, 2010

MH.IDDI AZZAN AWAOMBA WANANCHI WA HANANASIF WACHAGUE MAFIGA MATATU, KINONDONI

Mh.Iddi Azzan mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Kinondoni kupitia chama cha Mapinduzi akitoa sera zake kwa wananchi wa kata ya Hananasif, akiwaomba wamchague awe mbunge wa Jimbo hilo la Kinondoni ili wapate maisha bora, pia aliwataka wamchague Mh.Jakaya kikwete katika nafasi ya Urais ili aweze kushirikiana nae pamoja na Mgombea Udiwani wa kata hiyo Ndugu Tarimba Abbas.
Mh.Iddi Azzan akimnadi mgombea Udiwani Ndugu Tarimba Abbas wa kata ya Hananasif, katika uwanja wa kampeni wa kata hiyo Jana.
Ndugu Tarimba Abbas mgombea nafasi ya Udiwani kata ya Hananasif akitoa sera zake kwa wananchi wa Kata hiyo. awaomba wananchi wampe  kura nyingi sana Mh.Iddi Azzan na Mh.Jakaya Kikwete ili waendelee kuongoza nchi hii na kuwapatia Watanzania maisha bora.
Mh.Iddi Azzan akimkabizi kadi ya chama cha Mapinduzi mwanadada ambaye alijunga na chama hicho hivi karibuni.
Mh.Iddi Azzan akivishwa skafu na Chipukizi baada ya kuwasili kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Kata ya Hananasif.
Mh.Iddi Azzan akiwa amesimama baada ya kukaribishwa kwenye mkutano wa kampeni zake uliofanyika kata ya Hananasif.
Mh.Iddi Azzan akisimama na kujitambulisha kwa wananchi wa kata ya Hananasif baada ya watoto chipukizi kuta afanye hivyo walipokuwa wanawasilisha ujumbe kwake.
Mh.Iddi Azzan akiwaambia wananchi wa kata ya Hananasifu ikifika Tarehe 31 October "wanachukua wanaweka waaaa" baada ya kuambiwa aseme maneno hayo na Watoto Chipukizi.
Chipukizi watoto wakitoa ujumbe kwa wagombea Mh.Iddi Azzan na Ndugu Tarimba Abbas katika uwanja wa Kampeni Hananasif.
Chipukizi watoto wakitoa mkono wa salamu Kwa wagomba na Viongozi wa meza kuu ya mkutano uliofanyika Hananasif.

Kijana Macdonald akitoa mkono wa salamu kwa wagombea baada ya kutoka kuhutubia kwenye jukwaa la kampeni
Wananchi wakiwa wanashangilia juu ya gari katika uwanja wa mkampeni wa kata ya  Hananasif.

Watoto wakigombania kumsalimia Mh.Iddi Azzan baada ya kumaliza mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Hananasif, Kinondoni.


No comments:

Post a Comment