Friday, October 8, 2010

MH.IDDI AZZAN AITEKA KATA YA MZIMUNI

Mh.Iddi Azzan akiwapa sera wananchi wa kata ya Mzimuni katika uwanja wa Mtambani.
Katibu wa Vijana Mkoa wa Dar-es-salaam akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Kinondoni Mh.Iddi Azzan katika Uwanja wa Mtambani kata ya Mzimuni.
Mh.Iddi Azzan akimnadi Diwani wa Kata ya Mzimuni Ndugu Mohammed Chambuso wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Mtambani katika kata hiyo.
Chipukizi Mtoto ambaye anaitwa Mohamed akitoa Ujumbe kwa Wananchi akiwataka wakipe  kura nyingi chama cha Mapinduzi kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani.
Mgombea Udiwani Ndugu Mohammed Chambuso akiwa pamoja na kada wa CCM Ndugu Macdonald wakati wa kampeni  zilizofanyika uwanja wa Mtambani kata ya Mzimuni.
Mh.Iddi Azzan na Katibu wa Vijana na viongoze wangine wakiwa wanafurahia maigizo yaliokuwa yakionyeshwa mbele yao.
Muigiza wa kikundi cha Maigizo cha Mizengwe akitoa  mkono wa salamu kwa wagombea na viongozi wa chama. wakati wa kampeni zilizokuwa zinaendela kataka uwanja wa Mtambani kata ya Mzimuni.
Watu walikuwa wengi uwanjani.
ilikuwa hapatoshi mpaka kwenye miti Watu walipanda.
Wingi wa wananchi na wana CCM wakiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Mtambani, kata ya Mzimuni.

No comments:

Post a Comment