Friday, October 8, 2010

MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIWETE ASHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA IKULU.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata keki wakati wa sherehe ya kuadhimisha miaka 60 tangu kuzaliwa kwake pembeni yake ni Mkewe Mama salma Kikwete na mjukuu wao Karima wakishuhudia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimlisha kipande cha keki mkewe Mama Salma Kikwete wakati wa sherehe ya kuadhimisha kuzaliwa kwake miaka 60 iliyopita.Sherehe hizi zilifanyika katika viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete akimlisha keki mmoja wa wajukuu zake kwenye hafla ya kuzaliwa kwake iliofanyika katika viwanja vya taasisi ya WAMA.,kulia kwake ni Mama Salma Kikwete.
Rais Kikwete na Mkewe mama Salma Kikwete wakitakiana afya njema kwa kucheeers mbele ya wageni waalikwa usiku wa kuamkia leo,Rais Kikwete alikuwa akisherehekea siku yake maalum ya kuzaliwa kwa kutimiza miaka 60.
Mh.Jakaya Kikwete akitoa shukurani kwa wageni waalikwa waliofika kwenye hafla hiyo na kwa waandaaji pia wa shughuli nzima kwa usiku huo.
Mtoto wa Rais Kikwete,Ridhiwani Kikwete akimpa zawadi baba yake na pia kumpongeza kutimiza miaka 60 ya kuzaliwa kwake,kwenye hafla fupi iliofanyika usiku katika viwanja vya taasisi ya WAMA na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali.
Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete akimpa zawadi Mumewe,Mh Kikwete.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh Ally Hassan Mwinyi akiwa ameongoza na Mh Pius Msekwa wakimpa mkono wa pongezi Mh Jakaya Kikwete kwa kutimiza miaka 60 tangu kuzaliwa kwake.
Mh.Jakya Kikwete akiwa karibu na Mh.Iddi Azzan pamoja na wageni waalikwa wakiburudika na makamuzi live ya wana Sikinde.


No comments:

Post a Comment